Wednesday, May 22, 2013

East Africans in USA gear up for Massive Toronto Conference


Pastor Jared Mlongecha of the International Gospel Church in Chelsea, MA, USA

By Harrison Maina, AjabuAfrica.com,


BOSTON, MA_Dozens of Tanzanians, Kenyans Ugandans, Rwandese and other nationals from the east African countries in Boston and Kansas are planning to attend a major Christian revival conference to be held in Toronto Canada next month presided by renowned Tanzanian evangelist, Bishop Zachary Kakobe of Zachary Kakobe International Ministries.

Dubbed the “The Toronto Miracle Healing Crusade & Restoration Retreat”, the 5 day conference has also attracted the attendance by top world gospel musicians including Don Moen, Donnie Mcclurkin Martha Munizzi and the Krystal Brothers.

It is scheduled to start on Thursday June 20th to Sunday June 23rd at the Canada Tennis Rexall Center, a popular stadium that hosts major world Tennis tournaments.

According to Rev. Jared Mlongecha pastor of the International Gospel church in Chelsea, MA, who is the main coordinator of the conference, about 50 east Africans in Boston and about 60 from Kansas Missouri are planning to attend the unique event.

Pastor Mlongecha said that the believers will travel to Toronto in busloads as a group to minimize expenses and maximize the unique experience at the 5 day conference.The trip also includes a one day relaxation trip to the famous Niagra Falls a short distance from the crusade venue.

“This is a major conference. Bishop Kakombe has done tremendous work in the spiritual world leading many to experience healing, deliverance, signs and wonders. Barren women have conceived, cancers and tumors have been healed, real problems have been solved,” said Rev. Mlongecha during an interview with AjabuAfrica.com on the upcoming conference.

He added that there will also be a Restoration Retreat where singles, couples and the youth will be ministered to Bishop Kakobe.( View more details here >> )

“We expect massive restoring broken marriages and relationships, breaking the spirit of celibacy, bad habits, addictions and many more debilitating issues of life.”

At the end of the conference, the group plans to take a time off to visit the legendary Niagara Fall for sightseeing and general entertainment, Mlongecha leads the International Gospel Church in Chelsea that is frequented by worshippers from practically all the east African nations.

“However, we are welcoming other east Africans in the region who would like to attend the unique Toronto conference to join us so they can also be ministered to by Bishop Kakobe,” he added.

Pastor Mlongecha has been closely involved at organizing international conferences for Bishop Kakobe in many different countries including motherland Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, DRC and many others.

He said that the bishop has traveled in many other parts of the world including a sermon at the Yoido Full Gospel Church, an Assemblies of God church led by Dr. David Yonggi Cho in South Korea.

The church is considered to host the world's largest congregation with a membership of 1,000,000. (Wikipedia)

As the main coordinator for Bishop Kakobe’s international conferences, Rev. Mlongecha has been working together with a committee of pastors from different evangelical churches across Canada to organize the Toronto crusade.

According to Mlongecha, the trip to Toronto from Boston is a 9 hour drive and all the logistics have been worked out for all those who would like to accompany them for the conference.

The pastor said that conference attendees from the Boston region will take buses to Toronto at a cost of $120 per person for the roundtrip.

Plans have been worked out with the Toronto Airport Marriot Hotel, a 5 Star Hotel in Toronto where where four people can l share a room at a discounted rate of $35 a night per person.

After attending difference sessions and retreats at the conference, we will take a trip to the Niagara falls which is about 1 hour drive from the Rexall Center. There is no extra cost of this leisure trip to before we go back to our hotel for the final evening dinner.”
\
The trip has been generating a lot of excitement among many east African faithful from Boston, Kansas City, Kansas, Ohio, Michigan, and elsewhere in USA have contacted organizers with plans to attend the crusade.

This is a special kind of crusade that I will be attending together with my wife. We are looking forward to a great time with other believers,” said Rev. John Baker Katende, pastor of the global Evangelical church, a predominantly Ugandan church based in Burlington, MA.

Other east Africans reached by AjabuAfrica.com about the trip said that the trip is worth every penny as it provided a great opportunity to experience spiritual revival and taking a road trip to Toronto provides a break from the busy working schedules of most people who cherish a summer vacation.

“I will go for the trip because it provides me an opportunity to attend the crusade and take a little vacation with my family. I would also like to experience the Niagra falls in the company of people that I am familiar with. This is a great opportunity,” said Alex Kamau a Kenyan living in Boston.

For more information or to sign up for the trip, interested readers are requested to contact: Pastor Daniel Kungu (913) 850-4698 E-mail: pastor Kungu @ gmail.com

Alex Kamau (618) 509-1386. International Gospel Church (617)884-1951.

On the Net: https://bishopzacharykakobe.org/en/events/upcoming-events

Tuesday, May 21, 2013

Kwa Nini Bibi Harusi Hulia Siku ya Harusi?


Swali uliulizwa:

Hawa najiuliza, kwanini mabibi harusi wengi wanapenda kulia siku ya ndoa?

1. Jee! Ni uchungu au furaha kwa kupata mume?

2. Ni uchungu au kufaraha ya kuondoka mazingira ya nyumbani kwao?

3. Ni furaha ya kwenda kuanza kumiliki kitanda na mumewe mfululizo na
kwa muda anao upenda (lile tendo)?

3. Au wanaogopa fedheha kwa kuwa wanaolewa /anaolewa akiwa si bikra?

4. Ni uoga wa kuanza kulala bila nguo ya ndani akiwa kwenye ndoa na mumewe?

Kwa nini mabibi harusi wengi huangua vilio?!
Dada Leila Sheikh kajibu hivi:
Kwetu sisi uswahilini usipolia wafinywa na kungwi.
Seriously huwa tunalia kwa sababu tunaondoka kwa wazazi wetu na kwenda kujiunga na koo jingine.
huwa tunafundwa- "Mama Mkwe ndiyo Mama Yako sasa. Ba Mkwe ndiyo Baba Yako kuanzia leo. Hawa usiwachukulie kama mawifi au mashemeji bali ndiyo ndugu zako kuanzia leo. Mume akiwa kachacha, gongesha vikombe majirani wafikiri munakunywa chai kwa bajia. Chakula kikikosekana, hakikisha unachoma iliki ili majirani waamini unapika pilau. Mume akichelewa kurudi, mlaki mlangoni kwa tabasamu. Akikukaripia, mwimbie wimbo wa mapenzi "Sabalkheir (ishakuwa asubuhi anaporudi) Mpenzi, waonaje hali yako?".
Na kwa nini nisilie baada ya kuambiwa hivyo?Unaondoka kwenu ulipodeka wenda ugenini.
Leila Sheikh

Sunday, May 19, 2013

Rais Obama kutua Tanzania


President Barack Obama

 Kutoka Gazeti la Mwananchi

Rais wa Marekani Barack Obama ambaye anatarajiwa kudhuru Tanzania siku za hivi karibuni 
Kwa ufupi;
Akizungumza na Mwananchi Jumapili Profesa Ibrahim Lipumba ambaye ni mchumi kitaaluma, amesema kuwa ujio wa Rais Obama unaweza kuleta neema hasa kama atakuwa ameambatana na wataalamu wa masuala ya maendeleo.

Hii itakuwa ziara ya pili ya Rais Obama katika Bara la Afrika.
Dar es Salaam. Imeelezwa kuwa ujio wa Rais Barack Obama wa Marekani nchini, ni fursa nyingine kwa Tanzania kukuza uchumi na kuimarisha uwekezaji.

Akizungumza na Mwananchi Jumapili Profesa Ibrahim Lipumba ambaye ni mchumi kitaaluma, amesema kuwa ujio wa Rais Obama unaweza kuleta neema hasa kama atakuwa ameambatana na wataalamu wa masuala ya maendeleo.

Hii itakuwa ziara ya pili ya Rais Obama katika Bara la Afrika.
Ziara yake ya kwanza aliifanya wakati wa awamu yake ya kwanza madarakani, wakati ziara ya safari hii ni kipindi chake cha lala salama.

Rais Obama alianza rasmi awamu yake ya kwanza kama Rais wa Taifa kubwa, Januari 20, 2009, wakati ng’we yake ya mwisho ilianza Januari 21, 2013.

Rais Obama anatarajiwa kufanya ziara hiyo mwishoni mwa Juni mwaka huu, ambapo Tanzania itakuwa miongoni mwa nchi za mwanzo za Afrika Mashariki kutembelewa na kiongozi huyo.
Ziara ya Rais Obama inafanyika baada ya ziara ya Rais Xi Jiping wa China aliyeitembelea Tanzania Machi 28, mwaka huu, ambapo Tanzania ilikuwa nchi yake ya kwanza kuitembelea kwa Afrika tangu achaguliwe kuwa rais, Machi 14, 2013.

Akizungumzia ziara hiyo tarajiwa, Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Wananchi (Cuf), Profesa Ibrahim Lipumba ambaye ni mchumi, alisema amani, utulivu na uimara wa mfumo wa demokrasia ya vyama vingi kwa kulinganisha na nchi nyingine za jirani, vimechangia kuwapo kwa ziara hiyo.
Profesa Lipumba alisema pia ugunduzi wa rasilimali za asili kama vile gesi, mafuta na madini ya urani ni sababu nyingine iliyomfanya Rais huyo kuja nchini.

Hivyo aliwashauri viongozi wa Serikali kujipanga kwa ajili ya kufungua mlango huo mwingine wa uchumi na uwekezaji.

Alisema pamoja na hali hiyo pia kuna mambo ambayo yanaweza kuchafua taswira ya nchi kama vile ubovu wa miundombinu ya barabara, msongamano wa magari barabarani na msongamano wa meli bandarini wakati zikisubiri kushusha mizigo.

Jumatano ya wiki hii, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, John Kerry alitangaza mbele ya wajumbe wa Kamati ya Ushirikiano kati ya Marekani na Afrika, kwamba Rais Obama hivi karibuni atafanya ziara Afrika.

Ingawa Kerry hakutoa maelezo zaidi ya nchi gani za Afrika ambazo Rais Obama atazitembelea, lakini baadhi ya vyombo vya habari vya Nigeria vilieleza kiongozi huyo atafanya ziara Tanzania, Rwanda na Nigeria.

Kiongozi wa kwanza wa Afrika kukutana na Rais Obama tangu awe Rais wa Marekani, alikuwa Rais Jakaya Kikwete aliyekutana naye Mei 2009, Washington, Marekani.

Kwa nini ni Tanzania na Rwanda
“Kenya asingeweza kwenda kutokana na suala la Rais na Makamu wake kutuhumiwa kuhusika katika mauaji ya kimbari yaliyotokea baada ya uchaguzi mkuu 2007/2008, kwani msimamo wa Marekani ni kutaka wahusika wa vitendo vile wakamatwe na kufikishwa mahakamani. Hivyo kwake kuwatembelea watuhumiwa asingeeleweka,” alisema Profesa Lipumba.

Alibainisha kuwa Rwanda ina uhusiano wa karibu na Marekani na pengine suala la mgogoro wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) litachukua nafasi.

Kulingana na taarifa za Ikulu ya Marekani, Rais Obama alikuwa amepanga muda wake mwingi wa awamu ya pili ya uongozi wake kujihusisha na masuala ya Afrika.

Tanzia - Mzee Ally Sykes

The Late Mzee Ally Kleist Sykes
Mzee Ally Sykes amefariki hospitalini Nairobi.   Poleni wanafamilia wa Sykes. Baba yake marehemu Kleist Sykes alikuwa moja wa waanzilishi wa TANU.

May his soul rest in eternal peace. Amen.

*********************************************************************

FAMILIA YA SYKES INASIKITIKA KUTANGAZA KIFO CHA  MZEE WAO ALLY KLEIST SYKES  (PICHANI) KILICHOTOKEA LEO MEI 19, 2013  KATIKA HOSPITALI YA AGA KHAN JIJINI NAIROBI, KENYA,  ALIKOKUWA AMELAZWA.

MSIBA UKO NYUMBANI KWA MAREHEMU MBEZI BEACH JIJINI DAR ES SALAAM. MWILI WA MAREHEMU UNATARAJIWA KUWASILI JIJINI USIKU HUU.

MAZISHI YAMEPANGWA KUFANYIKA KESHO MEI 20, 2013 KATIKA MAKABURI YA KISUTU BAADA YA MWILI WA MAREHEMU KUSWALIWA KATIKA MSIKITI WA KIPATA WAKATI WA SWALAT ALAASIR.

HABARI ZIWAFIKIE NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI POPOTE PALE WALIPO.

Inna-na lillahi wa inna ilayhi raji'un. Hakika sisi sote ni waja wa Mwenyezi Mungu, na kwake tutarejea.
Surely we belong to Allah, and to Him shall we return.

Wednesday, May 15, 2013

Uke Yapotea Baada Ya Kufanya Mapenzi na Mwanaume Aliyeoa Kenya



Duh! Hii kali, huyo mganga wa kienyeji Kenya ana dawa kali sana.

Kuna dada fulani kutoka Ukambani, Kenya mwenye miaka 29. Alikuwa na mazoea ya kutembea na wanaume wa watu. Mke wa jamaa fulani kamwonya huyo dada kuwa ataathirika vibaya akiendelea kutmbea na mume wake.  Yule dada hakusikia na badala yake kaendelea kutembea na jamaa. Basi wiki hii baada ya kufanya kitendo na yule jamaa aliamka kwenda kukojoa (haja ndogo)....Akakuta uke/kuma yakeimezibwa kabisa!   Baada ya yule dada kuomba msamaha kwa yule mama, waliondoa ile dawa. 

Hii dawa inafaa sana!  Mganga huyo atatajirika!

Kwa habari kamili BOFYA HAPA:

Saturday, May 11, 2013

Happy Mother's Day!

Happy Mother's Day!



Nawatakia akina mama wote sikuukuu njema ya Akina Mama!

Friday, May 10, 2013

Polisi Kilosa Wakamatwa na Fuvu la Binadamu - Waliitumia kudai Rushwa


Kutoka Gazeti la Mtanzania!

Mei 10, 2013


JESHI la Polisi mkoani Morogoro limeingia kwenye kashfa nzito baada ya askari wake watatu na raia wanne kukamatwa wakiwa na kichwa cha binadamu. Tukio hilo lilitokea Mei 7 mwaka huu katika eneo la Mgudeni- Dumila wilayani Kilosa.

Inaelezwa kuwa polisi hao kwa kushirikiana na raia hao walikwenda nyumbani kwa mfanyabiashara Samson Mura na kutaka kumbambikizia kesi ya mauaji.

Mbali ya kubambikizia kesi hiyo, polisi hao wanadaiwa kuomba wapewe Sh milioni 25 na mfanyabiashara huyo ili wasimpeleke kituoni.

Wakizungumza na MTANZANIA jana, baadhi ya wananchi walisema wameshangazwa na askari hao ambao wawili ni wa Kituo cha Polisi Dumila na mmoja wa Kituo cha Polisi Mvomero.

Walisema siku ya tukio, polisi hao walifuatana na raia mmoja ambaye jina lake limehifadhiwa kwa ajili ya masuala ya usalama.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Mgudeni,Zaituni Kifutu alisema walishangazwa na tukio hilo.

“Tumeshangazwa mno na askari hawa… sijui walichukulia wapi mafunzo yao? Kama walibaini kuwapo tukio hili kwa nini hawakutaka kulifikisha kituoni?

“Inasikitisha mno, eti wao kwa kushirikiana na mfanyabiashara wanakwenda kudai kwa mwanakijiji mwenzetu wapewe Sh milioni 25… haiingi akilini hata kidogo wakamate mhalifu halafu washirikiane kwenda kuomba fedha.

“Tunaona na mazingira ambayo askari na raia huyo ambao walifika kwenye nyumba ya mfanyabiashara huyo, Samson Mura na kumtuhumu kukutwa na kichwa hicho si mazuri ni ya kutaka kumbambikizia kesi tu. Yaani inasikitisha jeshi kujaa uozo kiasi hiki,”alisema Kifutu.

Naye Musa Magisu alisema polisi hao walifika kwenye nyumba ya Mura na kufanya upekuzi ambao hata hivyo hawakuambulia kitu.

“Pamoja na kupekua kwa nguvu kubwa, hawakukuta kitu. Sisi tunamfahamu Mura ana silaha yake ambayo anamiliki kisheria,”alisema.

Alisema baada ya polisi hao kutoka nje ya nyumba walikwenda moja kwa moja kwenye gari lililokuwa limeegeshwa nje ya nyumba.

“Baada ya kufika kwenye gari, yule raia na wale polisi waliona kuna mfuko wa rambo chini na ghafla wakaanza kuuliza eti mfuko huu una nini na walipofungua wakakuta kuna kichwa cha binadamu.

“Yaani baada ya kukuta kichwa kile, walimuamuru mfanyabiashara yule atoe Sh milioni 25 lakini alikataa katakata akidai hajawahi kufanya tukio la aina hiyo,”alisema.

Alisema mpaka sasa hawajui kwa nini polisi ambao ni walinzi wa raia na mali zao, wamegeuka watu wa kumbambikizia kesi wananchi wasio na hatia.

Ofisa Upelelezi Msaidizi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Morogoro, Asifiwe Ulime alikiri kutokea tukio hilo na kusema mpaka sasa polisi hao wanashikiliwa kwa mahojiano zaidi.

Alisema hata yeye mwenyewe, alifika eneo la tukio na kushuhudia fuvu.

“Tunawashikilia polisi watatu na mwananchi mmoja kwa mahojiano ili watoe maelelezo ya kina juu ya tukio hili,”alisema.

Kutokana na hali hiyo, Ulime amewaomba wananchi wa Dumila kuwa watulivu wakati uchunguzi unaendelea.

Wednesday, May 08, 2013

Charles Ramsey Shujaa!

Charles Ramsey(43) wa Cleveland, Ohio amekuwa shujaa Marekani baada ya kumsaidia mama wa wa kizungu aliyetekwa miaka kumi iliyopita kutoroka katika nyumba ambako alifichwa.  Huyo mama ni Amanda Berry ambaye sasa ana miaka 27. Alitekwa akiwa na miaka 17 akitoka kazini.  Nakumbuka walitangaza kupotea kwake hadi hapa Boston.  Baada ya yeye na binti yake wa miaka 6 kutoroka polisi waligundua kuwa akina dada wengine wawili waliotpotea miaka mingi iliyopita walikuwemo ndani ya hiyo nyumba pia. Kwa vile walipotea muda mrefu watu walidhani wamekufa.  Kuna jamaa, Ariel Castro (52) na kaka zake wawawili waliokuwa wanawaficha na kuwabaka na kuwafanyia matendo ya ajabu! Baba wa mtoto wa Amanda ni Mzee Ariel.

Hao akina Castro wana asili ya Puerto Rico na MaRican wenzao wamekasirika na kusema wamewaibisha vibaya sana!  Wanyongwe!

Kwa habari zaidi BOFYA HAPA:


"Taifa Lina Nyufa" - Mh. Mbunge Zitto Kabwe



TAIFA LINA NYUFA

Na Mh. Mbunge Zitto Kabwe

NDUGU KABWE Z. ZITTO, MB – BUNGENI TAREHE 6 MEI, 2013


Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia leo katika mjadala huu muhimu sana.

Hapa Afrika kulikuwa kuna nchi, na bado ipo, inaitwa Ivory Coast. Ilikuwa ni nchi ambayo inasifika sana kwa amani na utulivu; na ilikuwa ni nchi ya kupigiwa mfano. Leo hii Ivory Coast imegawanyika vipande vipande. Ukienda leo Ivory Coast unakuta wanaoitwa Ivorite na wanaoitwa wageni ambao wazazi wao walienda Ivory Coast kufanya kazi miaka mingi sana. Lakini pili katika mgawanyiko huo kuna mgawanyiko mkubwa sana wa kidini kati ya watu wa Ivory Coast wanaotokea Kaskazini na watu wa Ivory Coast wanaotokea Kusini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa tuna Sierra Leone nchi ambayo wageni walikuwa wanakirimiwa katika hali ambayo haijawahi kutokea hapa duniani. Lakini leo Sierra Leone ina rekodi kubwa sana ya watu wenye ulemavu kwa sababu ya vita ya wenyewe kwa wenyewe.

Naomba nichukue nafasi hii kufuatia matukio ambayo yametokea hivi karibuni na hasa jana na siku zilizopita ninanukuu hotuba ambayo Rais wa Awamu ya Tatu Mheshimiwa Benjamin Mkapa aliitoa katika Bunge hili tarehe 4 Novemba, 1998. Alisema:

“Mr. Speaker, after three years of my presidency, I can dare to modify the words of famous Zanzibar maestro Siti Binti Saada by saying, Tanzania is a good country, let one who wishes to come do so. God has showered blessings on our country. It is a country of unity, peace, love, rejoicing and exciding generosity. It is a country of people who love equality and justice. Our national unity brings from our firm believe in equality of human beings before God and before the Law. A Unity reinforced by correct policies of national building. Policies based on the principles of social justice, peace, harmony and development for all. A unity which is extra sensitive to policies, statements behavior and actions which may sore seeds discard hatred and suspicious among Tanzanians”

Mheshimiwa Mwenyekiti sitatafsiri. Lakini naomba kila Mbunge ajiulize leo iwapo Rais Mkapa tukimpa fursa ya kuja kuhutubia Bunge hili anaweza akayatumia maneno haya tena? Hakuna mtanzania yoyote anayeweza kuthubutu leo kutumia maneno haya tena kwa sababu nchi yetu ina nyufa. Ina nyufa ambazo kwa kujua au kwa kutokujua sisi kama watu ambao tumepewa wajibi na wananchi wa kuitunza nchi hii na kuipeleka pamoja tumejikuta tukiingia katika kutoa kauli, maneno na vitendo ambavyo ni “irresponsible” vinavyopelekea kugawanya nchi; na yanayotokea sasa ni matumizi ya nyufa hizo.

NDUGU KABWE Z. ZITTO

Asubuhi hapa Mheshimiwa Lissu amesema, ametoa rekodi ya namna ambavyo wanasiasa wa chama kinachoongoza (CCM) wamekuwa wakitoa kauli dhidi ya vyama vya upinzani kuhusiana na masuala haya ya kidini. Wametoa mfano kuhusu chama cha CUF kilipoitwa chama cha waislam, wamekitolea mfano kuhusu CHADEMA kinavyoitwa mpaka sasa chama cha wakristo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, inawezekana ikawa ni rahisi sana tuka-“point fingers” kwa wenzetu nyie, ni rahisi sana; lakini CUF wakati wanaitwa ni chama cha waislam ambao walikuwa hawaitwi ni chama cha waislam hawakunyoosha mkono kupinga. Wakati CHADEMA kinaitwa cha cha Kikristo ambao hawaitwi hivyo hawakunyoosha mkono. Matokeo yakeni nini? Tumejenga hofu kubwa sana katika Taifa na hii ni lawama kwa wote. Wote kama nchi ili tuseme kwamba hapa tumekosea na tuanze upya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, adui anapokuja kwenye nyumba anaangalia ni wapi ambapo ni rahisi kamba kukatika. Tumeji-“expose”, tumejiweka wazi. Leo mtu anayetaka kuishughulikia Tanzania ata-deal na udini tu. Kwa sababu anajua watanzania hivi sasa wamegawanyika katika misingi hiyo. Jana limetokea tukio Arusha, angalia kwenye mitandao ya kijamii mara moja watanzania wenyewe kwa wenyewe na ukiangalia majina ya watu wanaojadiliana wanaanza kusemana kwa dini zao. Ndiyo hatari ambayo tumeifikia; na ndio anachokitaka adui. Ni hicho. Atakuja, wanaitwa “Agent Provacateur”, watapiga, mtabaki mnagombana ninyi. Tukiruhusu NYUFA hizi ziendelee hatutakuwa taifa. Ni lazima sote kwa pamoja tusimame imara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, waislam na wakristo nchi hii hawana chuki kwa sababu wanaishi pamoja, ni marafiki, ni ndugu na kama ingekuwa kwa mfano waislam wanawachukia wakristo waislam wangevunja makanisa au wangechoma makanisa au wangewalipua wakristo. Wakati wa tukio la Mwembechai ndipo ambapo Polisi waliingia mskitini wakaua watu, wanawake wakateswa kwenye magereza na kadhalika, watu wakakaa miezi mitano gerezani bila kushtakiwa lakini hapakuwa na mtukio yoyote ya namna hii. Waislam na wakristo wa nchi hii ni wamoja. Wananchi wetu ni wa moja lakini sisi viongozi kwa kutoa kauli ambazo ni “very irresponsible” tunawagawa watu wetu na ni lazima tukatae hali hii. Tunafanya nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima twende mbele. Kwanza ni lazima sasa Serikali ijenge utamaduni wa kufuatilia “grievances” zote ambazo wananchi wanazo bila kujali dini zao. Pili turuhusu watu kuwa huru kusema. Nimesikia hapa watu wanasema kwamba maandamano ni tatizo nakadhalika. Maandamano si tatizo, ukimzuia mtu kuandamana akiweka hasira zake kesho atafanya nini? Atatoka na bomu. Turuhusu “honest discussions” miongoni mwetu kama wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu ni lazima sasa tuseme ya kwamba ni marufuku kuwa na kauli za chuki “hate speeches”. Kama hatuna vipengele vya kisheria tutunge sheria kwa sababu kumekuwa na “hate speeches” nyingi sana katika hii nchi na hakuna hatua ambazo zinachukuliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, state, dola, ihakikishe inajiondoa kwenye shughuli za uendeshaji wa mambo ya kidini. Ijiondoe kabisa. Kwa mfano kuna lawama ya muda mrefu sana ya waislam kuhusu BAKWATA, Waislamu miaka mingi toka mwaka 1969 wakati Serikali imeunda BAKWATA wanalalamika. Leo hii Serikali ikitaka kuzungumza na waislam inafanya nini? Inaenda kuwaita BAKWATA. Hawana legitimacy ya waislam, hamtaweza ku-addres masuala ya waislam lakini ni rahisi sana kuweza kuongea na CCT kwa sababu CCT ni chombo ambacho kina uhuru wake. Kwa hiyo Serikali ijiondoe kwenye uendesheji wa shughuli za kidini. Hapa ndipo tutakapoweza kuhakikisha kwamba tunakuwa na nchi moja nchi ambayo ina amani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namaliza kwa kusema nchi hii si ya waislam peke yake, nchi hii si ya wakristo peke yake. Nchi hii si ya CCM au ya CHADEMA, CUF au ya NCCR-Mageuzi au TLP na kadhalika. Nchi hii ni moja, nchi hii ni ya Jamhuiri ya Muungano wa Tanzania. Lazima wote tusimame kuhakikisha tunailinda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru sana asante.