Wednesday, April 30, 2008

Kijana Edward Rupia anaomba Msaada Wenu


Wadau, kijana Edward Rupia, ana miaka 12.( Pichani yuko na Hasheem Thabit) Namfahamu tangu azaliwe. Wazazi wake ni waTanzania Godfrey na Bupe Rupia. Kwa sasa anakaa na mzazi moja tu, mama yake. Baba yake yuko Tanzania.

Naomba wadau wenye moyo msaidie kusudi aweze kwenda kuwa Student Ambassador, huenda ndo Obama wa kesho.

***************************************************************

March 27, 2008

Edward Rupia
27 Langen RD
Lancaster, MA

To Whom It May Concern:

My name is Edward Rupia, and I am a 6th-grade student at Browning Elementary School in Lancaster. I was recently interviewed and accepted to participate as a member of the People to People Student Ambassador Program to Holland this summer. The objective of the program is to promote international understanding while building leadership skills among America's youth. The 20-day experience includes meetings with government officials, interaction with other students my age, educational activities, and compete in basketball-sanctioned tournament.

I am currently seeking financial sponsors to help me with tuition, and hope I can count on your support. In case you haven't heard of People to People, please allow me to share some history with you. President Dwight D. Eisenhower founded the organization in 1956. He believed that if people from different cultures could come together in peace and friendship, so eventually would countries. Since its founding, People to People has launched many international programs, including Sister Cities and Project HOPE.

People to People Student Ambassadors are carefully interviewed and evaluated before their acceptance and I am honored to have been selected. Personally, I am looking forward to broadening my perspectives of the world and gaining a better understanding of Western European history. Upon my return, I plan to share my experience with schools and civic clubs in our community. As an Ambassador, I can also earn high school and college credit because of the many educational elements in my program.

The program tuition is $5,600, which includes all transportation, accommodations, meals and educational activities. I am asking any contributors to each donate any amount to help me reach my goal. Is it possible for you to assist me by making a contribution? Any amount of contribution would be appreciated. I will plan to give a speech and share my journal, photographs, and experiences with contributors upon my return.

My program tuition is due May 5, 2008. Check may be made payable to people to people ambassador. Please feel free to contact me at 978-413-0235 if you need more information. Your generous contribution would enable me to share in this wonderful opportunity. Thank you in advance for your consideration and support.

Sincerely yours,

Edward Rupia
Student Ambassador

Utamu wa Tunda la Kuiba

Wadau nimekuta haya mashairi JAMBO FORUMS. Yanafurahisha kweli.

*****************************************************************
Jamvini najikongoja,

Cheichei kwa pamoja,

Heko mlotoa hoja

'Sauti ya Shamba'

kwa kuleta hii hoja,

Naye 'Mwangwi wa Handaki' kajibu moja kwa moja,

Kaomba tumalizie Waridi chake kioja,

Nami nabinya vitufe kujibu hoja kwa hoja,

Tunda la kuiba tamu!


Tulia na utulize moyo wako,

Punguza kilio chako,

Kwani si wewe peke yako,

Hata wa pembeni yako,

Tuna kilema ka'chako,

Tunda la kuiba tamu!


Ingawaje nina tunda langu,

Lindani shambani mwangu,

Naliona kama nungunungu,

Linachoma kwa uchungu,

Nachelea la mwenzangu,

Nauona ulimwengu,

Si wangu ni wa wenzangu,

Nidokoe tunda tamu!


Tunda limenishangaza,

Kwa unono lapendeza,

Kwa deko lanipumbaza,

Lina ngozi yateleza,

Na macho yakulegeza,

Udenda nikachuruza,

Jino nikatumbukiza,

Tunda nikalibinyiza,

Jamani la kuiba tamu!


La kuiba tamu tunda,

Hiyo ndiyo yake inda,

Lau upepo ukipinda,

Akakufuma mlinda,

Tendo baya takutenda,

Kwa machozi utaenda,

Nenda ewe mwana kwenda,

Hapo tamu huwa chungu!


Wahenga wajisemea,

Yana tabu mazoea,

Tunda 'kishalizoea,

Sasa lishakupotea,

Tena umelikimbia,

Masikini la kuiba tamu!


Yana tabu mazoea,

Mengine 'takodolea,

Kwani tamu 'mekolea,'

Talinyemelea pea,

Kidole talinyoshea,

Nono tajichagulia,

Mate tajidondoshea,

Utamu jamani tamu,

unda la kuiba tamu!

Litabaki kuwa tamu!!!


By Palloma (Binti wa Kitanga)


***********************************************

Mzee Mwanakijiji Ajibu:


Tulia mwana nipange, majibu yangu niseme,

Tulia bila mawenge, hoja zangu mzisome,

Tulia miye nilonge, hili tunde nisiteme,

Tunda lile la jirani, hilo halina gharama!


Tulia nikuambie, uzuri wa tunda lile,

Tulia nisimulie, tunda hilo ni la kale,

Tulie nihabarie, na wewe hilo ukale,

Tunda lile la jirani, hilo halina gharama!


Tulia mwenye kuhoji, Bwana Bushiri kapanda,

Tulia la mwenye mji, hakuliacha kuvunda,

Tulia yeye mpaji, kalitunza hilo tunda,

Tunda lile la jirani, hilo halina gharama!


Tulia mimi nakiri, sikuingia gharama,

Tulia akisafiri, najinoma huku nyuma,

Tulia alfajiri, hadi wanapoadhama,

Tunda lile la jirani, hilo halina gharama!


Tulia kama mlevi, ndivyo ninavyosambua,

Tulia kama mvuvi, tunda ninalichambua,

Tulia silete gomvi, utamu nimeng'amua,

Tunda lile la jirani, hilo halina gharama!


Tulia hata samadi, wa kijiji sikuweka,

Tulia si ukaidi, mwenyewe naneemeka,

Tulia silipi kodi, la bure nalitamka,

Tunda lile la jirani, hilo halina gharama!


Tulia mwana nitame, kaditamati nafika,

Tulia msiniseme, ati nimeghafirika,

Tulia kisu kichume, na mchuzi kumwagika,

Tunda lile la jirani, hilo halina gharama!


Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)

Kibira Films watangaza seli ya DVD





In anticipation of the summer we are pleased to announce some price reductions on our existing movies. This is a good time for you to get your very own quality Swahili movies. Act now because these deals will not last forever.

Starting now: Bongoland I DVD can now be purchased at $12.99 was $15.00

Tusamehe DVD can now be purchased at $12.99 was 17.99

You can bundle both movies (Tusamehe and Bongoland) at $22.00CLICK HERE to order your copy today...

Gary Dourdan akamatwa na madawa ya Kulevya!

Gary Dourdan
Gary Dourdan Mugshot

Mcheza sinema, Gary Dourdan (41) amekamatwa na madawa ya kulevya ya aina mbalimbali huko Palm Springs, California. Polisi wanasema alikuwa amelewa vibaya shauri ya kutumia hayo madawa na alikuwa hajijui walivyomkamata.

Kwa kweli huko Hollywood habari hizi ni za kawaida ila huyo Gary anacheza kama mpelelezi, Warrick Brown, ambaye kazi yake ni kukamata wahalifu kwenye TV Show, CSI:Crime Scene Investigation! Ni aibu kubwa sana kwake. Watu walikuwa wanamheshimu sana na alikuwa anaalikwa sehemu nyingi kuongea na vijana kuhusu jinsi ya kuishi maisha safi bila kuingia kwenye nyayo za uhalifu.

Polisi wanasema walimkuta amelala ndani ya gari, taa inawaka ndani ya gari, na gari ilikuwa upande wa barabara isiyotakiwa. Walimkuta na madawa ya kulevya mbalimbali kama unga, heroin, vidonge na mengineyo.

Kwa habari zaidi someni:


Tuesday, April 29, 2008

Sinema - Paul Blart:Mall Cop

Mimi na Mcheza sinema, Jamal Mixon kwenye set ya Mall Cop
Mimi na Mcheza sinema, Jerod Mixon


Mcheza sinema, Kevin James
Mcheza sinema, Jayma Mays
Segway

Wadau, jana nilikuwa extra kwenye sinema, Paul Blart:Mall Cop ambayo itakuwa sinema ya vichekesho (Comedy). Nilishinda kwenye seti huko Burlington Mall siku nzima. Kuanzia saa 2:30 asubuhi hadi saa nne usiku (8:30am -10:00PM). Tulifanya kwanza scene ya arusi. Bwana arusi ni Kevin James na Bibi Arusi ni Jayma Mays. Kevin ndo mhusika mkuu wa hi sinema, yeye ndiye Paul Blart:Mall Cop.

Kwanza tulipiga scene tumekaa kwenye meza kama wageni waalikwa. Food Court ulikuwa umepambwa kama ukumbi wa arusi. Halafu walipiga scene kadhaa, wanafungishwa ndoa, busu, Bibi harusi kutupa bouquet, wahusika wakuu wengine wa sinema waki-react kwenye arusi. Halalfu walipiga scene za Bibi na Bwana arusi kuondoka wakiwa kwenye segways. Halafu tuliambiwa tucheze densi. Wimbo ulikuwa, 'Ain't No Mountain High Enough' ulikuwa unaimbwa na kaka yake Kevin James.

Mwisho walicheza densi wakiwa kwenye segways ndani ya gazebo. Hapo tuliambiwa tuzunguke gazebo. Ilitokea kichekesho wakati titi la Jayma ilitoka nje ya gauni la arusi. Watu walichecka walisema kumbe ana matiti feki. Yaani unaona kabisa ni mpira wa kupachikwa.
Basi, kuna kipindi tulikuwa tunapumzika. Akatokea mcheza sinema, Shirley Knight, ambaye anacheza kama mama yake Jayma Mays. Alikuja mezani kwetu alichukua kisu na kasema, "Naomba mtu anichome kisu!" Heh! Tulipigwa butwaa na kubakia midomo wazi. Alichukua kisu na kuanza kujichoma maeneo ya tumbo. Tukadhania huyo mama ni mwendazimu. Basi aliishia kucheka na kusema kavaa mapedi kusudi aonekana ni mnene maana siyo mnene hivyo. Hapo na sisi tulianza kucheka. Lakini kwa kweli tulishikwa na woga.

Kwenye scene ya mwisho ya arusi, mimi na mama mwingine mweusi tuliambiwa tusimame na Jamal Mixon. Nilifurahi kweli maana hapo chensi ya kuonekana vizuri kwenye sinema inakuwa kubwa kama uko na moja na wahusika wakuu wa sinema. Jamal utamkumbuka kwenye sinema kama, The Nutty Professor na Gridiron Gang.

Baada ya kumaliza scene ya arusi, tuliambiwa tubadilishe nguo. Halafu tulipiga scene ambayo tunakimbia. Jamaa anafoka, "Kuna mtu mwenye bastola!" Basi ndo tunakimbia kutoka nje ya mall. Karibu tukanyagane utadhani mtu alikuwa na bastola kweli.

Wakati tunasubiri kupiga hizo scene niliongea na Jamal na kaka yake Jerod Mixon. Kwa kweli ni vijana poa sana. Tuliongea kuhusu sinema za Hollywood na jinsi roles kwa ajili ya weusi ambazo ni za maana ni chache. Jamal alisema kuwa anatunga screenplays sasa akiwa hayuko kwenye sinema.

Kuona scene kutoka The Nutty Professor Bofya linki chini ni sinema ya kwanza ambayo Jamal alifanya wakati huyo ana miaka 14:

Filamu zinazowania tuzo Tanzania zatajwa!

Filamu zinazowania tuzo ya Vinara wa Filamu Tanzania zatajwa!

Filamu zilizoingizwa na watengenezaji wa filamu nchini kuwania tuzo za Vinara wa Filamu Tanzania 2007/2008 2007/2008 (Vinara Film Awards), zimetajwa.

Katika taarifa kutoka mratibu wa One Game Promotion inayoaandaa tuzo hizo, Khadija Khalili, iliyotumwa kwenye vyombo vya habari zaidi ya filamu sabini zinawania tuzo hizo.

Taarifa hiyo ilizitaja filamu hizo kuwa ni Crying Silently (Kilio Moyoni), Kolelo, Mwanahiti, Zawadi ya Fisadi, Oloboni na Layoni, Mmera (Jando) na Nyamaume.

Nyingine ni Sumu ya Moyo, Segito, A Point of no Return I, A Point of no Return II, Dar to Lagos, Cross my Sin na Penina.

Pia zimo Habari Kubwa, Fake Pastor, Chite Ukae, Surprise, Stranger, Fungu la Kukosa, Sea Man, Mzee wa Chabo, Donda Ndugu, I Love You, Miss Bongo I, Miss Bongo II, Revenge, Behind the Scene, na My Wife.

Taarifa hiyo ilizitaja nyingine kuwa ni My Sisters I, My Sisters II, Machozi ya Nyamoma, Silent Killer, My Wife, Greena, Kiapo cha Damu, Valentine, Mwana Pango, Utata, Yolanda, Picnic, Uwanja wa Dhambi, Misukosuko II, Copy, Lugha Gongana, Mtoto wa Mjini, Nyuma ya Pazia, Macho Mekundu, Tanzia, Welcome Back, Karibu Paradiso, Swahiba, The Game of Love I, The Game of Love II na The Game of Love III.

Nyingine ni Mahabati, Security, Itunyama, The Body Guard, Agano la Urithi, Ndani ya Gereza, Simu ya Kifo, My Heart, Malipo ya Kisasi I, Malipo ya Kisasi II, Mpasuko wa Moyo I, Mpasuko wa Moyo II, Kisasi na Diversion of Love.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa, majaji watakutana wiki ijayo kuanza kuziangalia tuzo hizo.
Taarifa hiyo ilisema kuwa filamu zinazowania tuzo hizo ni zile zilizokamilika kutengenezwa Januari 2007 mpaka Machi 31, 2008.

Vipengele vinavyoangaliwa na majaji katika filamu hizo ni Filamu Bora ya Mwaka, Muigizaji Bora wa Mwaka wa Kiume, Muigizaji Bora wa Mwaka wa Kike, Muigizaji Bora Chipukizi wa Mwaka wa Kiume, Muigizaji Bora Chipukizi wa Mwaka wa Kike, Muongozaji Sinema Bora wa Mwaka, Mchekeshaji Bora wa Mwaka, Mwandishi Bora wa Filamu na Mtunzi Bora wa Filamu.

Vingine ni Filamu Bora ya Kutisha, Muigizaji Mwandamizi Bora wa kike (supporting actor), Muigizaji Bora Mwandamizi wa Kike, Adui Bora kwenye Filamu, Wimbo Bora wa Mwaka (Sound Track), Mhariri Bora wa Filamu ambao wote watapata tuzo na zawadi.

Pia itatolewa tuzo ya heshima kwa wale waliotoa mchango wao kukuza sanaa nchini.
Tuzo hizo zinazotarajiwa kutolewa mwishoni mwa mwezi Mei zimedhaminiwa na bia ya Ndovu Special Malt, Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na Global Publishers.

MK Music Galaxy - Muziki kutoka Bongo

Habari,

Ule wakati tulio usubiria sasa umefika, Website ya pekee itakayo jishughulisha ktk kuutangaza muziki wa Tanzania ipo jikoni na ina karibia kuiva.
Unataka kusikiliza muziki wa nyumbani? Basi watembelee wajuzi wa fani hii kupitia www.mkmusicgalaxy.com kwa miziki mipya na ya kizamani uburudike roho yako.
Nawatakia siku njema.
Kind Regards,
Support Department

MK MUSIC GALAXY - Exploring the Tanzanian Music.
Part of MK GROUP OF COMPANIES (T) LTD - http://www.mkgroupltd.com
Website: http://www.mkmusicgalaxy.com
Tel: +44 - 752 - 792 - 9234

Sunday, April 27, 2008

Kwame Nkrumah wa Ghana

Kwame Nkrumah na mke wake na machifu huko Ghana siku ya Januari 20, 1963


Ule ukumbi mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, unitwa Nkrumah Hall. Ilipewa jina hiyo kwa heshima ya rais wa Kwanza wa Ghana, Kwame Nkrumah.

Ghana ilikuwa nchi ya kwanza ya weusi kupata Uhuru barani Afrika. Ilipata Uhuru mwaka 1957 kutoka Uingereza. Mwaka 1960, Nkrumah alitangaza kuwa Ghana ni Jamhuri. Mwaka 1964, alisema yeye ni rais wa maisha ya nchi hiyo. Alikataza vyama vyote vya siasa isipokuwa chama chake.

Mwaka 1966 alipokuwa safarini China, alipinduliwa. Alikufa akiwa exile nchini Romania mwaka 1972.

Nkrumah alikuwa na ndoto ya bara Afrika kuwa, UNITED STATES OF AFRICA. Wadau mnadhani kuwa bara Afrika inaweza kuwa nchi moja kama majimbo ya Marekani? Tulivyo na lugha na utamaduni tofauti na ukabila sidhani kama itawezekana kwa sasa. Labda baada ya miaka 200!

Kwa habari zaidi za Kwame Nkrumah someni:

http://www.thenagain.info/WebChron/Africa/Ghana.html

http://news.bbc.co.uk/onthisday/hi/dates/stories/march/6/newsid_2515000/2515459.stm

http://www.africanews.com/site/list_messages/16337

Saturday, April 26, 2008

Update - Mtoto Kichaa akutwa na kichwa cha mtoto


UPDATE - April 29, 2008

Mama mzazi wa mtoto salome yohana aliyechinjwa majuzi akilia kwa uchungu wakati akisaidiwa kuweka udongo kwenye kaburi la binti yake wakati wa mazishi tabata segerea jioni hii.

Picha kwa hisani ya issamichuzi.blogspot.com

**********************************************************


KUTOKA MICHUZI BLOG:

Katika kufuatilia tukio la huyu kijana pichani kukutwa na kichwa cha msichana leo asubuhi kule muhimbili, globu yenu imethibitishiwa kwamba jana usiku msichana mdogo alipotea nyumbani kwao tabata.

Inasemekana leo asubuhi ndugu wa marehemu walikuta kiwiliwili kitupu cha msichana huyo karibu na nyumbani kwao na wakaita polisi ambao wakaupeleka hospitali ya taifa ya muhimbili kwa uchunguzi. huko ndiko kichwa kinachosadikiwa kuwa cha kwake kikakutwa na huyu kijana kwenye geti la chuo kikuu cha tiba cha muhimbili ambapo mlinzi alimkamata.

Afande charles mkumbo, mkuu wa upelelezi kanda ya ilala, amethibitisha yote hayo usiku huu na kwamba kichwa hicho ni cha mtoto salome yohana mwenye umri wa miaka kati ya miaka 3 na 4 na kijana huyu ametambulwa kama ramadhani mussa na anashikiliwa na polisi yeye na mama yake kwa kutuma za kukutwa na kichwa cha mtu kwa kile kilichosemwa kuwa ni mambo ya kishirikina.

Kijana mussa mwenye umri wa miaka 12 inasemekana pia amewahi kukumbwa na mikasa mingine, ikiwa ni pamoja na kuanguka toka paa la kanisa la assemblie of God la msasaani analoongoza mh. getrude rwakatare. inasemekana baada ya mkasa huo ambapo alikuwa na mwenzie wa umri kama yeye walipelekekwa kupimwa akili muhimbili na kuachiwa baada ya kuonekana wana akili timamu.

Mtoto Kichaa Muhimbili - Onyo Picha Zinatisha!





Nimepokea haabri hii ya kusikitisha. Inaelekea ni habari ya kweli. Naomba mlioko Dar mthinitishe kama ni kweli. Je, huyo mtoto kichaa anaitwa nani? Huyo mtoto marehemu ni nani?

Kama ni kweli ni lazima wakubwa walihusika! Wakamatwe wahusika wote na wapewe adhabu ya kifo!
******************************************

On 4/26/08, Dr. M Wrote

Dakika chache zilizopita kumetokea tukio la kusikitisha hapa MPL Muhimbili. Askari mmoja alimsimamisha mtoto wa miaka kama 9 hadi 11 akiwa amebeba kichwa cha mtoto mzuri kama wa miaka mitatu. Kijana yule akatoa kichwa mfukoni na kuanza kula live. Nikifika home nitawatumia picha. Ajabu sana



Kijana mla kichwa cha mtoto alisema kuwa anapeleka zawadi kwa shangazi yake yuko IPPM (siyo psychiatry). Ni kweli tukio hili la kusikitisha sana limetokea.Kichwa ni cha mtoto wa kike mzuri (binadamu), it seemed to be fresh.


Alidai anapeleka zawadi hiyo kwa shangazi yake yuko psychiatry!Mara baada ya kukamatwa, alianza kula kile kichwa live !!! !!! Hata hivyo baadhi ya mashuhuda wanasema aliyekamatwa aliwahi kulazwa psychatry unit.Kwa kuaangalia umbo lake, naye ni mtoto pia; hivyo nina walakini kuwa ni psychiatric patient (unless ana childhood neuropsychiatric/ neurodevelopmental disorders).



Mbona amekuja Muhimbili na si kwingineko. Mfano, angekamatwa maeneo ya Ubungo ama kwingineko; akataja Muhimbili psychiatry tungesikuwa na maswali mengi sana. Kwa upande mwingine, kula kichwa LIVE mbele ya kada mnasi inatia walakini kwa binadamu wa kawaida mwenye akili timamu.



Wazazi/ walezi wa watoto hao (aliyetafunwa na aliyetafuna) wako wapi?Wana maelezo yapi?Pamoja na hayo, kiwiliwili kiko wapi? Kikipatikana chote (kuanzia shingoni hadi miguuni) kitatoa baadhi ya majibu.Polisi wa kutosha (magari mawili) wameondoka na kijana huyo uchunguzi (forensic investigation) unaendelea.



AMINI USIAMINI, NI KWELI YAMETOKEA.

Miaka 44 ya Muungano

Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, akichanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar kama ishara ya muungano rasmi, April 26, 1964. Siku hiyo Tanzania ilizaliwa.

*****************************************
Wadau nawauliza hivi - huo udongo uko wapi?

Mnahabari kuwa jina la Tanzania ilipatikana katika mashindano. Watu waliombwa wapeleka majina ya nchi mpya. Tanganyika + Zanzibar. Karibu tuitwe TANGIBAR!

Leo namwomba Mungu kuwa tuendelee kujivunia uTanzania wetu. Tuendelee kukaa kwa amani na utulivu na tuendelee kuwa mfano na nyota barani Afrika. AMEN

Friday, April 25, 2008

Umoja Church Texas


Habari zimetoka kwa Pastor Absolom wa Umoja Church, Dallas Texas:

Kwa niaba ya kanisa lenu la Umoja,tunapenda kumkaribisha kila moja wenu katika mkutano wa kesho ambao mtumishi wa Mungu Mama Newstar Ngereja atahudumia.
Mbali na mkutano huu, tunapenda pia kutangaza msiba wa BIBI BUPE MWAIJANDEM ambae ni bibi mzaa mama wa mwanajumuia, na mshirika wa kanisa la Umoja dada BAHATI na WINNIE. Msiba huu umetokea jana huko nyumbani Mbeya, Tanzania. Tunaomba wanajumuia watakaoweza kufika kanisani kwa ajili ya ibada na kuwafariji wafanye hivyo kesho siku ya jumamosi saa moja jioni.Kwa watakaoweza kuwapigia simu na kuwafaraji wanaweza kufanya hivyo kwa namba hizi;214 779 4469,214 576 8903, 214 989 8778,214 554 7381. Kwa direction ya kanisa angali juu ya tangazo letu.
Umoja

Boston Casting wanatafuta Extras

Kuna mdau aliniomba linki ya kuwa Extra. Hii hapa ni moja ya Casting Agencies za Boston.

**************************************************************

From Boston Casting

EXTRAS WANTED

If you are interested in being an extra in the ” Untitled Kevin James Film” please click on “talent application”, complete the form and upload 2 photos. With a free profile we can consider you for movie extra work. The software provider, Agency Pro, also offers valuable marketing tools at a fair price if you chose to make this investment in your career. The free account is enough to get you considered for extra work.

If you are already have an account please update it if you are “union” or “nonunion”, your age range, and make sure there is a photo up. This will help us when we are searching for you !

Thursday, April 24, 2008

Wesley Snipes Ahukumiwa Kifungo - Miaka Mitatu!


Jamani, leo nimejua ubaguzi bado upo nchi hii. Wesley Snipes amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu kwenye gereza la serikali (federal). Kisa hakulipa kodi aliyostahili kulipa! Denzel Washington alikuwa mahakamani akitoa shuhuda kuhusu jinsi Snipes alivyo mtu mwema. Pia Woody Harrelson alitoa shuhuda. Snipes mwenyewe alimwomba hakimu amwonee huruma! Lakini wapi! Jaji kampa kifungo cha juu kabisa miaka mitatu. Alisema awe mfano kwa wengine!

Ninaamini angekuwa mzungu kama Tom Hanks au Tom Cruise angepewa probation, au kifungo cha siku chache au miezi michache.
Marekani lazime ulipe kodi. Kama hulipi utakamatwa tu. Kama si leo basi hata baada ya miaka!

Wadau mnasemaje?
Kwa habari zaidi someni:

Ndoa ya Star Jones na Al Reynolds yavunjika!

Star Jones kabla hajapunguza uzito na baada ya kupunguza
Arusi ya Star Jones na Al Reynolds 2004


Star Jones na Al Reynolds wakiwa kwenye Honeymoon

Star Jones na Al Reynolds baada ya Star kupunguza uzito


BEFORE AND AFTER


Haya leo nimekuwa umbea. Nimesikia habari kuwa Star Jones na mume wake Al Reynolds wanaachana. Kwa kweli mambo ya kuachana ni mambo ya kawaida hapa Marekani, lakini hii imekuwa habari kubwa.

Kama mnakumbuka walivyofunga ndoa ilikuwa habari kubwa kweli. Yaani Star Jones wakati huo alikuwa ni moja wa wanawake wa ile show, THE VIEW. Alikuwa anapendwa kweli na watazamaji.. Watu walivyosikia anaolewa kwa mara ya kwanza akiwa na miaka 42 walifurahi kweli ingawa walisema huyo mume wake anacheza upande mwingine (anapenda wanaume wenzake). Sasa baada ya kutangaza ndoa, alikuwa anatangaza details mpaka chupi atakayovaa mpaka watu wakaona kinyaa.

Mara baada ya kuolewa kwake alianza kupungua uzito, kawa mbaya wengine walisema kawa kama kinyago, halafu alitolewa kwenye THE VIEW. Alikataa kusema alipunguza uzito kwa njia gani. Kumbe alifanyiwa opresheni ya kupunguza tumbo. Watu walimchukia kwa vile alificha siri yake kwa miaka mitatu.

Sasa wanaachana. Nikitazama picha za Star kabla hajaolewa na sasa namwona mtu mwingine na alivyo sasa.
Hivi ni kwa nini mara nyingi watu wakifunga ndoa ya kifahari ndoa haidumu? Utakuwa watu walifunga ndoa simple lakini zinadumu miaka na miaka na wanapendana hasa.

Wadau mnasemaje?
Kwa habari zaidi someni:





Mchele umekuwa Adimu Marekani!


LOH! Haya sasa ni makubwa! Mchele umekuwa adimu Marekani, mpaka maduka yana weka 'limit' ya kiasi ambacho unaweza kununua. Nilikuwa nimesika fununu wiki iliyopita lakini sikutaka kuamini.

Mchele hasa ambao sasa umekuwa haba ni zile Basmati (pishori) na Jasmine (ya kunukia). Sehemu zenye wahindi wengi ndo wanaumia. Hebu fikiria watu wapenda madishi ya wali kama sisi waafrika na wahindi tukianza kukosa! Si itakuwa balaa! haya tuanze kuzoea pasta (spaghetti). Utakuwa kama enzi za mwalimu na miezi 18 (miaka 18). Sidhani kama hali unaweza kuwa mbaya kiasi hicho lakini.

Kwa kweli ni jambo la kushangaza sana kusikia uhaba wa chakula. Hata hivyo ni watu ambao wali ni chakula chao kikuu ndo wanaanza kuona uchungu. Bei umepanda mno. Hata hivyo bei ya vyakula kwa ujumla umepanda.

Yaani nikienda supermarket siku hizi nasikia hata wazungu wanalamika kuhusu bei ya chakula. Bei ya cereals, mikate, mayai, maziwa, nyama umepanda. Pia bei ya petroli umepanda mno . Na mimi nasema ukisikia mzungu analalamika basi unajua kweli hali umekuwa mbaya!

Hayo matatizo ni Asante Bush na vita yake isiyo na maana!

Naomba Obama achaguliwe kuwa raisi!

**********************************************************

Skyrocketing rice prices has Sam's Club limiting sales
4-24-08

(CNN) -- Retail chain Sam's Club will limit the sale of large quantities of rice amid a dramatic increase in the global price of rice.

Sam's Club will limit customers to four 20-lb. bags of jasmine, basmati and long-grain white rice.

The store will limit customers to four 20-lb. bags of jasmine, basmati and long-grain white rice, the company said in a statement. Its restriction mainly will affect businesses that buy rice in bulk, but the company said "a typical Sam's Club Business Member does not buy more than 80 pounds of rice in one visit."

"We currently have plenty of rice for Sam's Club members," the statement said. "This temporary restriction does not apply to retail-sized rice for sale in Sam's or elsewhere at Wal-Mart stores."

The restriction does not apply in Idaho and New Mexico.

Sam's Club -- a division of Wal-Mart Stores Inc. -- has 593 wholesale locations in the United States and more than 100 abroad, in countries such as Brazil, Canada, China and Mexico.
Food prices have soared worldwide in recent months, leading to violence in some developing countries.

"In just two months," World Bank President Robert Zoellick said this month, "rice prices have skyrocketed to near historical levels, rising by around 75 percent globally and more in some markets, with more likely to come."

Wednesday, April 23, 2008

Sinema - This Side of the Truth

Ricky Gervais akidirect scene. Leo alikuwa amevaa nguo hizo hizo, nadhani ana suruali 20 and sharti 20 za aina moja.
Nguo nilizovaa kwenye scene.
Hii ni sehemu ya seti. Hapo eti ni theatre inaonyesha sinema ya chanzo cha magari. Hebu tazama vizuri...hiyo siyo sinema hall ni benki. Ila set designers wameipamba kusudi ionekane kama sinema hall kwa nje.
Hapa crew wanafungasha kusudi waende zao nyumbani.

Leo nilikuwa extra kwenye sinema, THIS SIDE OF THE TRUTH. Stelingi wake ni mwingereza Ricky Gervais. Inapigwa Lowell, Massachusetts na Andover, Massachusetts. Tulikuwa Downtown Lowell, kwenye benki.

Crew wake wengi wanatoka Uingereza. Basi ilikuwa kichekesho watu walikuwa wanalalamika kuwa wanshindwa kuwaelewa wakiongea. Kweli kama umezoeza kiMarekani, kusikia Kiingereza halisi ni shida. Nilikuwa nawatafsiriwa wazungu niliokuwa nao. Wanauliza kasema nini? Nami najibu kasema hivi, na wao wanasema "Oh!". Nami nikasema huenda na sisitukiongea anapatashida kutuelewa.
Picha chache hizi kutoka seti. Haturuhusiwi kupiga picha kwenye seti. Hizi nilipiga baada ya kumaliza shoot. Leo nilikuwa mpita njia, natembea nyuma ya Ricky Gervais. Lakini hasa walitumia gari yangu. Walibadilisha plates. Nikatoka holding (wanapopumzika extras) na kwenda kwenye seti, sikutambua gari yangu mpaka niliona permits zangu kwenye dirisha.

Wanasema wataniita tena. Wiki ijayo nitakuwa kwenye sinema, Mall Cop tena.

Tuzo za filamu za Vinara zaiva!

PRESS RELEASE FROM ONE GAME:

Tuzo za filamu za Vinara zaiva!

Zoezi la ukusanyaji wa filamu zitakazoshiriki katika kinyang'anyiro cha Tuzo za Vinara wa Filamu Tanzania lilimalizika rasmi Ijumaa iliyopita ya Aprili 18, 2008 ikiwa ni hatua ya kwanza kabla ya kufanyika kwa onesho la utoaji wa tuzo hizo.

Akiongea nasi mratibu wa tuzo hizo zinazotolewa na kampuni ya One Game Promotions ya jijini Dar es Salaam, Khadija Khalili alisema kuwa, wamefanikiwa kupokea filamu zipatazo sabini na mbili kwa ajili ya kushiriki katika tuzo hizo kwa mwaka 2007/08.

"Zoezi la ukusanyaji wa filamu lilifanyika kwa wiki kadhaa, ambapo watayarishaji wa filamu walitakiwa kuchukua fomu katika vituo vilivyopangwa na kuzirejesha katika ofisi za Baraza la Sanaa Tanzania (Basata) pamoja na nakala za filamu zao," akasema.

Akaelezea zaidi kuwa, kukamilika kwa hatua hiyo ya ukusanyaji wa filamu hizo, ndio mwanzo wa hatua nyingine katika kuelekea kupatikana kwa wasanii watakaofanikiwa kutwaa tuzo hizo kwa mwaka huu.

Bi Khalili akaongeza, baada ya kupokelewa kwa filamu hizo, jopo la majaji litazipitia na kuibuka na majina matano katika kila 'kategori' na baadaye kusubiri hadi siku ya onesho la kutolewa kwa tuzo hizo kwa ajili ya kutambua atakayeibuka na tuzo kwa kila 'kategori'.

"Siku hiyo zitatolewa tuzo ishirini pamoja na tuzo ya heshima kwa msanii aliyetoa mchango mkubwa kwa sanaa hiyo nchini, hivyo tutakuwa na 'kategori' kumi na tisa zitakazokuwa na majina matano-matano, ambapo mmoja wao atatwaa tuzo," akafafanua.

Tuzo zinazowaniwa ni Filamu Bora ya Mwaka, Muigizaji Bora wa Mwaka wa Kiume, Muigizaji Bora Mwaka wa Kike, Muigizaji Bora Chipukizi wa Mwaka wa Kiume, Muigizaji Bora Chipukizi wa Mwaka wa Kike, Mwongozaji Bora wa Filamu wa Mwaka na Mchekeshaji Bora wa Mwaka.
Nyingine ni Mwandishi Bora wa Filamu, Mtunzi Bora wa Filamu, Filamu Bora ya Kutisha, Muigizaji Mwandamizi Bora Kike, Muigizaji Bora Mwandamizi wa Kiume, Adui Bora wa Filamu, Mhariri bora wa Filamu na Tuzo ya Heshima.

Wadhamini wakuu wa tuzo za Vinara ni Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia kinywaji chake cha Ndovu Special Malt pamoja na Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC). Onesho la tuzo hizo linatarajiwa kufanyika Mei 30 mwaka huu.

Tuesday, April 22, 2008

In Memoriam Prof. Henry Damson Kadete

Prof. Henry Damson Kadete
1954-1995
(Former Head of Electrical Engineering Dept. UDSM)

It's been 13 years today since you passed away. You are deeply missed by your wife, Chemi, an your sons Camara & Elechi, your sisters, brothers, nieces and nephews and friends. You will always be remembered. We miss you.

REST IN ETERNAL PEACE.

Tazama Mechi Hapa!

Dada Subi ameniletea linki hii:

*********************************************

Samahani kwa kuchelewa kuleta tangazo (nilikuwa najihudhurisha mbele ya liwali asinisahau kwenye ujira)ni hivi, nimebandika link hapa: http://nukta77.com/soccer.aspx mtu kuweza kuchagua pa kutizamia mechi za michezo mbalimbali ikiwemo huu wa soka/futiboli la leo (Liverpool vs Chelsea)

Kwa wale washamba wa vijiji vya USAgara/USA river na vitongoji vyake, huu ndiyo wakati mzuri wa kwenda sambamba na walioko Tz
Subi

Mazishi ya Ditopile

Rais Jakaya Kikwete. akiweka udongo kwenye kaburi la marehemu ditopile leo huko kinyerezi
Baadhi ya waombolezaji kwenye mazishi ya Marehemu Ditopile

Picha kutoka Michuzi Blog

Marehemu Kepiteni Ditopile Ukiwaona Athumani Mzuzuri amezikwa leo heo Kinyerezi, Dar es-Salaam.

Mola ailaze roho yake mahala pema peponi. AMIN.

Akuta Mamba Jikoni!


Huko Florida, bibi moja mwenye miaka 69, alimkuta mamba mwenye urefu wa futi nane jikoni kwake.

Sikiliza alivyoaomba msaada 9-11 hapa: 9-11 operator anamwuliza siyo kenge kweli?


Huko Florida kuna tatizo kubwa mamba. Ni protected species yaani wanalindwa hivyo ni marufuku kuwaua. Matokeo yake wamezaliana na wamakuwa wengi. Tukio za mamba kudhuru na hata kuua watu zimeongezeka huko Florida.

AFRICA/AFRIKA


Sisi ni waafrika. Je, tunajua nini kuhusu bara Afrika? Ni continent ya pili kwa ukubwa duniani. Ina madini kibao, maziwa, kuna nchi zenye rutuba, na nchi zenye ukame. Kuna nchi 53. Pia Afrika ina sifa nyingi zaidi. Wanasema kuwa binadamu wa kwanza walitokea bara Afrika, hivyo kila mtu dunia hii (hata wazungu) ana asili ya Afrika.

Leo jiulize unajua nini kuhusu bara letu Afrika.

****************************************************************


Africa
From Wikipedia, the free encyclopedia

Area
30,221,532 km² (11,668,598.7 sq mi)

Population
922,011,000[1](2005, 2nd)
Density
30.51/km² (about 80/sq mi)

Countries


Languages
African Languages and many others

Time Zones
UTC-1 (Cape Verde) to UTC+4 (Mauritius)

Africa is the world's second-largest and second most-populous continent, after Asia. At about 30.2 million km² (11.7 million sq mi) including adjacent islands, it covers 6% of the Earth's total surface area, and 20.4% of the total land area.[2] With about 922 million people (as of 2005)[3] in 61 territories, it accounts for about 14.2% of the world's human population.


The continent is surrounded by the Mediterranean Sea to the north, the Suez Canal and the Red Sea to the northeast, the Indian Ocean to the southeast, and the Atlantic Ocean to the west. There are 46 countries including Madagascar, and 53 including all the island groups.

Africa, particularly central eastern Africa, is widely regarded within the scientific community to be the origin of humans and the Hominidae tree (great apes), as evidenced by the discovery of the earliest hominids and their possible ancestors, as well as later ones that have been dated to around seven million years ago – including Sahelanthropus tchadensis, Australopithecus africanus, A. afarensis, Homo erectus, H. habilis and H. ergaster – with the earliest Homo sapiens (human) found in Ethiopia being dated to ca. 200,000 years ago.[4]

Africa straddles the equator and encompasses numerous climate areas; it is the only continent to stretch from the northern temperate to southern temperate zones.[5] Because of the lack of natural regular precipitation and irrigation as well as glaciers or mountain aquifer systems, there is no natural moderating effect on the climate except near the coasts.

Kwa habari zaidi za Afrika someni:


Monday, April 21, 2008

Kitanzini Iringa


Kuna baadhi yenu mliotaka kujua zaidi ya kihistoria kuhusu Kitanzini, Iringa. Pichani Mzee Nzowa bado anakumbuka mahala hasa uliposimama mti uliotumika na Wajerumani kuwanyongea Wahehe. Mahala hapo palijulikana kama Kitanzini.
Aliyefikishwa hapo alifungwa kitanzi shingoni na kuning'inizwa hadi kifo. Utotoni Mzee Nzowa alikua akiuona mti huo ingawa watu hawakuendelea kunyongwa hapo baada ya Mwingereza kuingia nchini.
Mti huo wa kihistoria anadhani ulikatwa miaka ya 50 wakati wa kutengeneza barabara za mitaa. Hadi hii leo eneo hili linajulikana kama Kitanzini. Kwenye nchi za wenzetu wangeweka haraka mnara wa kumbukumbu ili kuitunza historia kwa vizazi vijavyo.

Kipanya Kasema...

Translation:

Kipanya (Rat Character) - If in Nyerere's time the decided to do this I don't think you'd have anything left to harvest.

Kifo cha Ditopile


Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete wakimfariji mjane wa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Marehemu Ukiwaona Ditopile Mzuzuri huko nyumbani kwake Upanga. Kulia ni Mariam Ditopile mtoto wa marehemu na nyuma ya Rais ni mtoto wa Rais, Rashid Chodo Kikwete. Aliyesimama karibu na Mama Salma Kikwete ni ndugu wa marehemu ambaye jina lake halikuweza kutambulika mara moja

Maziko ya Mheshimiwa Ditopile ambayo yalikuwa yafanyike Aprili 21,2008 huko Kinyerezi sasa yatafanyika Aprili 22. Jana Aprili 20 maiti yake iliondolewa hospitali ya mkoa wa Morogoro na kupelekwa hospitali ya Jeshi Lugalo kwa hifadhi.Pichani jeneza lenye mwili wa marehemu Ditopile likiingizwa katika gari ya wagonjwa la jeshi kikosi cha Pangawe, Morogoro. Picha nyingine ni Rais Jakaya Kikwete akimpa salamu za pole mke wa Ditopile nyumbani kwake Upanga hapo Aprili 20,2008.


Picha kutoka Lukwangule Blog

Habari Kutoka Michuzi Blog


ALIYEKUWA Mkuu wa Mkoa wa Tabora Kepteni Mstaafu Ukiwaona Ditopile Mzuzuri aliyefariki jana Aprili 20,2008 majira ya saa 3:00 katika Hotel ya Hilux iliyopo Mkoani Morogoro anatarajiwa kuzikwa kesho huko Kinyerezi, pembezoni mwa jiji la Dar, maeneo ya Segerea.
Mamia ya waombolezaji wamefurika nyumbani kwa mareehemu mtaa wa Mindu, Upanga, Dar, kujiunga na familia ya marehemu katika kuomboleza kifo hicho ambacho kimeacha watu wengi midomo wazi.

Marehemu Ditopile alifikia katika hoteli ya Hilux ,Morogoro akitokea Tabora akiwa safarini kuelekea Dar es Salaam kwa mapumziko akiwa ameambatana na mkewe mdogo,Tabia.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa hoteli hiyo Joseph Kitambi, Ditopile alifika hotelini hapo Aprili 18, majira ya saa 5:30 usiku,ambapo alipatiwa chumba No.106.

Kitambi alisema Aprili 19,majira ya saa 5:00 usiku watumishi wa hoteli hiyo wakati wakifunga shughuli zao za huduma, Ditopile alikuwa bado hajarudi hotelini kutoka kwenye shughuli zake ambazo amekuwa akizifanya kwa muda wote tangu kufika hotelini hapo.

Akifafanua zaidi Mkurugenzi huyo alisema, Aprili 20 majira ya saa 2:30 asubuhi mkewe Tabia alitoa taarifa ya kuzidiwa kwa mumewe na kuomba msaada ambapo wahudumu walifika katika chumba chake na kumwangalia na kukuta akiwa amelala kwenye kochi,na alionekana kuwa ni mtu asiyejitambua,na kutoa taarifa kwenye hospitali kuu ya Mkoa kwa msaada zaidi.

Mkurugenzi huyo aliiambia habari leo kuwa marehemu alifariki kabla ya kupata kifungua kinywa cha asubuhi ambacho hutolewa na hoteli hiyo kuanzia saa 12:30 asubuhi hadi majira ya saa 4:30.
Alisema kuwa wauguzi wa hospital walifika katika hoteli hiyo,na kumchukua kwenye gari,akionekana kama mtu ambaye ameshafariki,na kumpeleka hospitalini kwa ajili ya kufanya uchunguzi zaidi.

Hata hivyo Mkurugenzi huyo alidai kwa kipindi chote ambacho Ditopile amekuwa katika hoteli hiyo,alionekana kuwa ni mtu aliyekuwa akisumbuliwa na maradhi,kutokana na mwili wake kudhoofu na nyuso kutokuwa na uchangamfu.

Aidha alidai kuwa wakati wafanyakazi hao wanautoa mwili wake nje kwa kushirikiana na madaktari waliofika kutoka hospitalini,walikuta mswala wa kuswalia,ambapo mkewe alidai kuwa mumewe aliamka alfajiri na kuswali swala ya asubuhi,kabla ya mauti kumkuta.Baada ya mwili huo kufikishwa hospitalini Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa Dkt.Meshack Masi alisema alipokea taarifa kutoka kwenye uongozi wa hoteli hiyo,iliyoeleza kuwa Ditopile amezidiwa hivyo wanahitaji msaada haraka.

'Kweli tulipokea taarifa hizo…walikuwa wakiomba msaada haraka…na sisi tulituma gari pamoja na wauguzi mara moja kwenda pale Hilux hoteli na kumleta hapa hospitalini'alisema Daktari Masi.

Hata hivyo Dkt.Masi alisema baada ya wauguzi kufika hotelini hapo,na kuuona mwili wake waligundua kuwa ameshafariki na kuubeba mwili wake na kuupeleka hospitalini hapo na kuulaza wodini grade 1, kwa ajili ya kuudhibitisha,kabla ya kuupeleka kwenye chumba cha kuhifadhia maiti.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro Thobias Andengenye alisema kuwa marehemu alipotoka mkoani Tabora alifika Mkoani Morogoro na kwenda Wilaya ya Mvomero kwa ajili ya kukagua mashamba yake yaliyopo kwenye eneo la Mgongola akiwa na mkewe mdogo Tabia kabla ya kufika Morogoro Mjini ambapo alipata malazi.

Aliongeza kuwa baada ya kukagua mashamba yake marehemu aliondoka Wilayani Mvomero na kuja Morogoro Mjini ambapo alifika majira ya saa 3 usiku na kufikia kwenye hotel ya Hilux iliyopo Mjini hapo kwa ajili ya kupata malazi ambapo alipewa chumba No.106.

Alisema marehemu aliitumia siku ya Aprili 19,kutembelea ndugu na jamaa zake kabla ya kurudi nyumbani kwake Jijini Dar es Salaam,na kudai kuwa alirudi hotelini hapo majira ya saa 12 jioni,ambapo alitarajia kuondoka Aprili 20 kurudi nyumbani kwake.

Katika ziara ya marehemu ya kutembelea na kusalimiana na ndugu zake,pia alipata wasaa wa kumtembelea Chifu Kingalu Mwana Banzi wa 14 wa kabila la waluguru.

Kwa upande mwingine mdogo wake na Marehemu, Selemani Mzuzuri,alipohojiwa alisema hana lolote la kuzungumza na kueleza kuwa bado ana majonzi mazito ya kifo cha kaka yake,hivyo hataweza kuzungumzia jambo lolote.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Meja Jeneral mstaafu Said Kalembo ambaye alifika hospitali ya mkoa wa Morogoro akizungumza na waandishi wa habari alisema kwamba mwili wa marehemu unatarajiwa kuchukuliwa na gari la jeshi na kusafirishwa kuupeleka kwenye chumba cha kuhifadhia maiti kwenye hospitali ya Jeshi ya Lugalo iliyopo Dar es salaam.

Marehemu Ditopile, ambaye pia aliwahi kuwa Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM, amewahi pia kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma,Lindi na Tabora kabla ya kukabiliwa na kesi ya Mauaji bila kukusudia.

Sunday, April 20, 2008

Ditopile Afariki!


Habari kutoka Tanzania zinasema Ditopile Ukiwaona Mzuzuri amefariki dunia leo asubuhi katika hoteli moja huko Morogoro. Habari za kuaminikia zinasema kuwa Ditopile alikuwa anatazama TV ndipo kapata Heart Attack na kufa.

Kesi ya mauji ya Ditopile, ambayo Ditopile alimwua dereva wa daladala pale njia panda ya Bagamoyo Rd. ilikuwa isikilizwe hivi karibuni.
Mola ailaze roho yake mahala pema peponi. AMIN.

***************************************


BREKING NYUUUZZZZZZ

HABARI KUTOKA MOROGORO ZINASEMA ALIYEKUWA MKUU WA MKOA WA TABORA UKIWAONA ATHUMANI DITOPILE AMEFARIKI DUNIA LEO ASUBUHI KATIKA HOTELI MOJA MJINI HUMO.

JUHUDI ZINAFANYWA KUJUA CHANZO CHA MAUTI YAKE. UONGOZI WA HOSPITALI YA MKOA IMETHIBITISHA KIFO HICHO.
**************************************
Habari kutoka Ippmedia.com
Ditopile allegedly guns down daladala driver 2006-11-06

Police in Dar es Salaam are holding Tabora Regional Commissioner, Capt (rtd) Ukiwaona Ditopile Mzuzuri for allegedly shooting to death a commuter bus driver. Dar es Salaam Special Zone Police Commander Alfred Tibaigana told a news conference yesterday that Ditopile, who once served the government as deputy minister, allegedly shot Hasani Mbonde (33) in the head, killing him instantly.
According to Tibaigana, police are holding the regional commissioner, as investigations into the killing continues. He said Ditopile, who has been in the public service for many years, having served as RC in a number of regions, allegedly shot the bus driver at around 7.pm, at the junction of Kawe and Bagamoyo roads in Kinondoni District on Saturday.
Tibaigana said Mbonde, a resident of Kawe Mzimuni, was driving a commuter bus an Isuzu Journey with registration number T788 ACC, plying between Ubungo and Tegeta. Detailing on the incident, he said the commuter bus had collided with a Prado vehicle with registration number T816 AJT which was being driven by Nasoro Mohamed (42) a resident of Kijitonyama.
Ditopile was a passenger in the Prado.
The RPC said Ditopile was heading to Bagamoyo from Dar es Salaam, with another passenger whose name could not be immediately be obtained. He said preliminary investigation shows that shortly after the collision, Ditopile’s driver alighted from his vehicle, to establish the extent of the damage.
He discovered a minor damage at the rear of the vehicle.
However, Ditopile also got out of the car to assess the damage, went straight to the commuter bus driver and ordered him out of his vehicle. The driver allegedly refused to budge and shut the door and window of the bus. ”At this juncture, Ditopile drew a pistol and used it to knocked on the window of the bus, insisting that the driver should come out,” Tibaigana explained.
He said in the course of the wrangle, Ditopile allegedly fired at the driver through the glass window and killed him on the spot. Tibaigana said the body of the deceased is being preserved at the Muhimbili National Hospital mortuary. Prior to his appointment as Tabora RC, Ditopile, popularly known as ’Dito’ served as deputy minister in the then Communication and Transport ministry and as RC for Kigoma, Lindi and Coast Region. He once served as Ilala legislator and member

Saturday, April 19, 2008

Jambo Forum T-Shirts












April 18, 2008


In regards to: T-Shirts for sale


To All JamboForums:

Hello everyone! I want to let you all know that there will soon be T-Shirts available for sale with our JamboForums logo on them. The T-Shirt is a 100% ring spun 6.1 oz cotton T-shirt that will be available in several different colors. The sizes available will be S-4XL. The colors that we have right now are red, black, white, and charcoal. This is a 100% cotton T-Shirt that is made by Port and Company, a Port Authority brand. The logo will appear on the left chest of the garment and will be in turquoise and white as shown on the web site. We will have the first T-Shirts available for sale starting the first week of May.

Price will be determined shortly. Shipping and handling will vary according to your location. At a later date we will also be offering an Egyptian Cotton Polo and hats with the same logo.

Also we are looking into getting products with less price for our people at home.
You can make your payment through Paypal or send your money order to:

Mohamed Ali
P.O. Box 105973
Jefferson City, MO 65110-5973
USA.

We would appreciate your interest and any feedback that you may have. Any suggestions for future products or colors available would be also greatly appreciated.

Any other questions, please direct them to me, I will be more than happy to answer them for you as much as I can.
Thank you,
Mwazange

Moto Shule ya Boarding Uganda







Huko Afrika ni kawaida kupeleka watoto boarding (shule ya kulala) ili wapate elimu. Huko Uganda wiki hii watoto wa kike 19 walipoteza maisha yao baada ya bweni lao kuchomwa moto. Polisi Uganda wanasema kuwa moto uliwashwa maksudi (Arson). Bweni hiyo ya shule ya msingi Budo, ilikuwa inalaza wasichana 58.

Aende motoni huyo aliyewaua hao mabinti!!! Walikuwa nio watoto wa shule ya msingi wenye miaka 9 hadi 12 tu. Kwa kweli kuna watu wenye roho ya kutu katika dunia hii. Sijui walimkosea nini huyo aliyeamua kuwaua!

Kwa sasa polisi Uganda wameshilikia walinzi tisa wa shule na matron.

**********************************

4-19-08

(AP) Ten people being held in connection with a fire that killed 19 Ugandan schoolgirls are all school employees, a senior police official said Saturday.

Nine guards and a matron are being held on suspicion of negligence, said the officer, who asked for anonymity because he was not authorized to comment on an ongoing investigation.

The officer said police suspect that Monday's fire at Budo junior school was started by arsonists. Witnesses reported a loud bang as the building burst into flames. The doors to the dormitory had been locked from outside.

Young survivors spoke of struggling to climb through tiny windows as their sleeping quarters filled with smoke.

Police are following two leads involving disgruntled school staff, the officer said. They have offered $3,000 for information.

The fire was the third fatal school fire in Uganda in two years.