Thursday, December 31, 2015

Heri ya Mwaka Mpya!

Nawatakia wadau wote Heri ya Mwaka Mpya!

Mkesha wa Mwaka Mpya DMV

 Mama wa mitindo Asya Idarous Khamsini akihesabu sekunde zilizoslia kuelekea mwaka mpya kwenye sherehe ya mkesha wa mwaka mpya 2016 iliyofanyika Lanham, Maryland siku ya Alhamisi Desemba 31, 2015 iliyoandaliwa na Jumuiya ya Watanzania DMV na kuwakutanisha wana DMV na familia zao wakiwemo marafiki kutoka majimbo mengine huku wengine wakiokea Tanzania. PICHA NA KILIMANJARO STUDIO
Wafuangaji champagne wakiwa tayari kama kikosi cha mizinga wakisubilia sekunde zilizobaki kuingia mwaka 2016 kuachia mizinga yao ikiwa ni sehemu yakusherehekea mwaka mpya wa 2016.
 Mama wa mitindo Asya Idarous Khamsini akifuahia kuuona mwaka mpaya, wapili toka kulia ni Rais wa Jumuiya ya Watanzania DMV Bwn. Iddi Sandaly pamoja na Asha Hariz (kulia) wakifurahia kuuona mwaka 2016.
WanaDMV wakikumbatiana kama familia moja na kupongezana "tumeuona mwaka 2016"
 Wanafamilia wakipongezana.
 Ni furaha ya mwaka mpya
Wanafamilia wakiwa katika picha ya pamoja kusherehekea kuuona mwaka,

Ni 2016 hiyo ni furaha kwa kwenda mbele.
Kwa picha zaidi bofya HAPA

Saturday, December 26, 2015

Mzee Njemba Atoweka Nyumbani kwake Magomeni, Ndugu Zake Wanamtafuta

Ndugu na jamaa wanatarifiwa kwamba Bw. Hemed Mzee Ibrahim "Njemba" (pichani)  ametoweka nyumbani kwake Magomeni Makuti mtaa wa Mchinga namba 22 jijini Dar es salam toka siku ya Alhamisi tarehe 24/12/2015. 
Alionekana mara ya mwisho kwenye msikiti wa Magomeni Makuti muda wa alasiri alipokwenda kuswali, akiwa kavaa balaghashia (kama hiyo pichani), shati la light purple, suruali ya bluu na kandambili za bluu. Baada ya hapo hakurudi nyumbani kwake na hadi sasa hajulikani alipo. Mzee Njemba hupendelea kutembelea Magomeni Makuti.
Wanafamilia wanaomba mwananchi atayebahatika kumuona atoe tarifa kwa mkwewe Yusuf  anayepatikana katika namba 0784 606 262.
Wanatanguliza Shukurani za dhati kwa wote na kumuombea salama mzee wao.


Friday, December 25, 2015

Krimasi Njema!

Nawatakia wadau wote Krismasi Njema!

Saturday, December 19, 2015

Afrika Haikuwa Maskini


Two Congolese Warlords Jailed


Germain Katanga



Thomas Lubanga



ICC Sends 2 Convicted Warlords to Congo Prison

   THE HAGUE, Netherlands (AP) - The International Criminal Court has sent two militia leaders convicted of committing war crimes in the Democratic Republic of Congo to that country to serve the remainder of their prison sentences.

   The court announced that Thomas Lubanga and Germain Katanga were transferred to a Congolese prison on Saturday.

   Lubanga was sentenced in 2012 to 14 years for using child soldiers in his militia during fighting in the mineral-rich eastern region of Ituri. Katanga was sentenced in 2014 to 12 years for crimes including being an accessory to murder.

  Katanga's punishment was reduced by appeals judges and he is due to complete his sentence Jan. 18.

  

Friday, December 18, 2015

Walioghushi Vvyeti ili Kupata Kazi Serikalini, Kiama Chao Hiki Hapa!



PICHANI JUU: Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki (Mb) (kushoto), akitoa maelekezo kwa Watumishi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu-UTUMISHI.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki (Mb) ameiagiza Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu-UTUMISHI kuwachukulia hatua watumishi waliobainika kutumia vyeti visivyo vyao kupata ajira Serikalini.

Mhe. Kairuki aliyasema hayo jana alipotembelea Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu–UTUMISHI ikiwa ni muendelezo wa ratiba yake ya kutembelea Idara/Vitengo vya Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma.

“Watumishi wote waliobainika kupitia Mfumo Shirikishi wa Malipo ya Mishahara ya Watumishi wa Umma (Payroll) kutumia vyeti visivyo halali kwao wachukuliwe hatua stahiki” Mhe. Kairuki amesema.

Aidha, Mhe. Kairuki amemtaka Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu-UTUMISHI Bw. Emmanuel Mlay kutafuta Ufumbuzi wa kumalizana na tatizo la watumishi wanaotumia vyeti vya kughushi.

“Muwasilishe vyeti vyao Baraza la Mitihani kwa ajili ya uhakiki na baada ya uhakiki muwachukulie hatua stahiki watumishi wanaoonekana kutumia vyeti visivyo halali kwao” Mhe. Waziri alisisitiza.

Naye, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu-UTUMISHI Bw. Leonard Mchau alisema kuwa Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma imehakiki jumla ya watumishi 704 ambao kati ya hao watumishi 219 baada ya vyeti vyao kuhakikiwa na Baraza la Mitihani wamegundulika kuwa waliajiriwa kwa vyeti vya kughushi.

Bw. Mchau aliongeza kuwa baadhi ya watumishi hao walioonekana kughushi vyeti ili kujipatia ajira Serikalini wamekimbia vituo vyao vya kazi.

Bw. Mchau aliwaasa wananchi kuepuka mchezo wa kughushi vyeti ili kujipatia ajira Serikalini.

“Ni kosa la jinai kughushi vyeti kwa lengo la kujipatia kazi hivyo endapo utagundulika umeghushi vyeti utachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria za nchi.”  Bw. Mchau alifafanua.

Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma inaendelea na zoezi la uhakiki wa vyeti kwa Watumishi wote wa Umma nchini na matarajio ni kuwahakiki watumishi wote.


***************************************************
 KUTOKA HABARI LEO

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki, ameiagiza Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu (Utumishi) kuwachukulia hatua watumishi waliobainika kutumia vyeti visivyo vyao, kupata ajira serikalini.

Kairuki amesema hayo jana alipotembelea idara hiyo katika muendelezo wa ratiba yake ya kutembelea Idara/Vitengo vya Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma.
“Watumishi wote waliobainika kupitia Mfumo Shirikishi wa Malipo ya Mishahara ya Watumishi wa Umma (Payroll), kwamba wametumia vyeti visivyo halali wachukuliwe hatua stahiki,” amesema Kairuki.

Amemtaka Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimali watu Utumishi, Emmanuel Mlay kutafuta ufumbuzi wa kumaliza tatizo la watumishi wanaotumia vyeti vya kughushi.

“Muwasilishe vyeti vyao Baraza la Mitihani kwa ajili ya uhakiki na baada ya uhakiki muwachukulie hatua stahiki watumishi wanaoonekana kutumia vyeti visivyo halali kwao,” alisisitiza.
Naye, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Usimamizi wa RasilimaliwatuUtumishi, Leonard Mchau, alisema kuwa Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma, imehakiki watumishi 704 na kati ya hao, watumishi 219 baada ya vyeti vyao kuhakikiwa na Baraza la Mitihani, waligundulika waliajiriwa kwa vyeti vya kughushi.

Hata hivyo, Mchau aliongeza kuwa baadhi ya watumishi hao waliobainika kughushi vyeti ili kujipatia ajira serikalini, wamekimbia vituo vyao vya kazi. Mchau aliwaasa wananchi kuepuka mchezo wa kughushi vyeti, ili kujipatia ajira Serikalini.

“Ni kosa la jinai kughushi vyeti kwa lengo la kujipatia kazi, sasa endapo utagundulika umeghushi vyeti, utachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria za nchi,” alifafanua Mchau. Kwa sasa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma inaendelea na uhakiki wa vyeti kwa watumishi wote wa umma nchini mpaka kila mmoja atakapohakikiwa.

Thursday, December 17, 2015

Term Limits Lifted for Rwanda

By IGNATIUS SSUUNA
Associated Press

   KIGALI, Rwanda (AP) - The head of Rwanda's electoral commission said late Friday partial results show Rwandans have voted to lift term limits in order to allow President Paul Kagame extend his rule.

   More than 98 percent from 21 out of 30 districts, representing 70 percent of registered voters, voted to lift term limits for Kagame, Mbanda Kalisa said. Kagame's supporters celebrated the announcement in the capital, Kigali.

   Kagame, 58, is ineligible to run in 2017 because the Rwandan constitution limits a president to two terms. But if Rwandans approve the referendum, Kagame would be able to run for an additional seven-year term and then two-five year terms, which means he could possibly stay in power until 2034.

Rwanda President Honourable Paul Kagame

 Kagame became president in 2000 after being Rwanda's de facto leader since the end of the country's genocide in 1994. He is credited with stabilizing the country and promoting economic growth after the mass killings, but critics say he is an authoritarian ruler who does not tolerate opposition and he is accused of human rights abuses.

   Rwanda's political opposition criticizes the referendum as undemocratic and the U.S., a key Rwandan ally, has opposed Kagame's bid to stay in power.

   The Chairman of the National Electoral Commission Mbanda Kalisa said partial results will be released later Friday.

   Many of the 6.4 million registered voters are expected to participate in the referendum.

   Kagame voted at Rugunga polling station in the capital, Kigali, accompanied by his wife and daughter.

   "What is happening is people's choice. Ask people why they want it," he said maintaining that it's the wish of the Rwandan people that he extends his term. He said he would announce his candidature "any time."

   Ninety-two per cent of Rwandans want President Paul Kagame for third term, according to a survey conducted by Ipsos, a global research firm, that was released this week.

   "President Kagame is a hero and statesman like former Tanzania President Julius Nyerere," says Dan Gatera, a voter in Nyamata, east of the country. "The constitution should not be used to limit presidents who have talents."

   Western diplomats voiced concerns about the vote. The European Union is worried that the opposition was not given adequate time to campaign against the referendum, said Michael Ryan, head of the EU delegation to Rwanda.

   "There should have been adequate time for debates, and educating people about the changes made in the constitution," Ryan told journalists.

   The Democratic Green Party of Rwanda is the only opposition party which rallied Rwandans to vote against changing the constitution to extend presidential term limits.

   Erica Barks-Ruggles, the U.S. Ambassador to Rwanda, said she is concerned because the referendum was organized very quickly.

   The move to change Rwanda's constitution was prompted by a petition signed by more than 3.7 million people. The petition was endorsed by the Senate and the lower house of Parliament last month and later by the country's Supreme Court.

   If Rwanda's term limits are changed and Kagame runs again, he will join a growing list of leaders in East and Central Africa whose governments have prolonged their rule by changing the limits on presidential terms.

   In 2005, Ugandan lawmakers changed that country's constitution, allowing President Yoweri Museveni to seek re-election in 2006 and 2011. He is running again in 2016.

   Neighboring Burundi has political unrest that started earlier this year when President Pierre Nkurunziza run and won a third term that many oppose saying it goes against the two five-year term limit imposed by the constitution.

   There have also been protests in Congo over efforts by President Joseph Kabila, who has been in power for 15 years, to prolong his time in office.

  

Wednesday, December 16, 2015

Nunua Tiketi ya Ndege Kwa Njia ya Installments Kupitia Tuzola



Tuzola ni kampuni ya waTanzania wanaoishi Marekani.  Kama huna hela  kamili ya kununua tiketi ya ndege unaweza kununua kwa kulipa kiasi awali, na baadaye ulipe hela iliyobaki (installments).  Kama unakaa Marekani unaelewa vizuri mambo ya kulipa bili kwa installment.

Saturday, December 12, 2015

Namba za Simu za Kuripoti Wanaofuja Hela za Serikali!



Maana ya MAGUFULIFY!


Uvaaji wa Chupi - Afya ya Uzazi



Na Mdau Joyce Masika

Leo naomba nikukumbushe somo la Afya ya uzazi. Somo hili litafafanua faida na hasara au madhara yatokanayo na uvaaji wa nguo za ndani hasa Chupi.
Uvaaji wa chupi kihistoria ulianza karne ya 19 baada ya uvumbuzi wa viwanda na mapinduzi yake yaliyoambatana na mapinduzi ya teknolojia.
Enzi za mama zetu na babu zetu uvaaji wa chupi haukuwepo hapa Tanzania. Uvaaji wa chupi uliletwa na wamisionari na wakoloni wakati wanaleta dini Africa. Kabla ya hapo waafrica hatukuwa na utamaduni wa KUVAA chupi.
Mtoto akizaliwa hakuvalishwa chupi kamwe kama ilivyo Leo.
Mwanamke pia enzi hizo alikuwa havai chupi. Mwanaume naye pia alikuwa havai chupi? Watu wote walikuwa hawavai chupi. Mwanamke alikuwa hachuchumai chini pindi akijisaidia kutokana na kwamba hawakuwa wanavaa chupi hivyo wakitaka kujisaidia haja ndogo walikuwa wanasimama tu na kupanua miguu na kuanza kukojoa.
Nyakati za leo ambapo uvaaji chupi kwa wanaume na wanawake uko juu sana kuanzia watu tunapokuwa watoto wadogo hali ya Afya ya viungo vya uzazi imeendelea kuwa mbaya sana. Yafuatayo ni baadhi ya madhara ya kuvaa chupi :

1. Magonjwa ya "Urinary tract infection" au UTI hayataisha kwako.

Hii hasa ni kwa wanawake wanavaa nguo nyingi kwa wakati mmoja na kwa muda mrefu zaidi ya saa kumi. Unavaa chupi, lakini tight, suruali ya jinzi, nk halafu unashinda na hizo nguo kuanzia asubuhi unapoenda kazini hadi saa mbili usiku unaporudi home. Hiyo ni hatari sana.
Mwanamke anayefanya kazi zinazompasa kuwepo kazini zaidi ya masaa 8 namshauri asiwe anavaa chupi kabisa. Chupi ivaliwe nyakati za hedhi tu. Kama hauko kwenye siku zako vaa suruali tu bila chupi. Au vaa underskirt pekee yake kwa ndani na ndoo uvae nguo yako ya kawaida. Hii itakuepusha na kuugua UTI. Ukiacha sababu za ngono UTI husababishwa na bacteria wanaopendelea mahali penye unyevu na joto. Kwa hiyo mwanamke akivaa nguo nyingi bacteria hao hujipatia joto la kutosha kuzaana.
Mwanamke ni vyema ukaepuka kuvaa nguo za kubana mwili sana ili kuepukana na uwezekano wa kupafanya ukeni pawe na joto sana na ikitokea bacteria mmoja tu akaingia humo atazaa haraka sana na kujikuta UTI inakuwa rafiki yako. Vaa sketi bila chupi au kama kuvaa suruali ni lazima hakikisha unavaa suruali peke yake. Jizoeze tu utazoea. Na ukizoea kuvaa nguo bila chupi utainjoi sana.

2. Magonjwa ya kuvu au fungus hayatakoma kwako.


Bado niko kwa wanawake, kama nilivyoeleza mwanzo hapo magonjwa ya fungus yanasababishwa pia na kuvaa chupi kwa muda mrefu. Chupi inayovaliwa kwa zaidi ya saa 8 lazima italeta ukungu au uvundo sehemu nyeti. Huo uvundo waweza kuleta fungus ukeni. Fungus za ukeni hazina tofauti na zile za miguuni kwa wanaume wanaovaa viatu kwa muda mrefu bila usafi miguuni wa kutosha.
Chupi inakuwa kama socks za wanaume. Mwanamke avaae chupi muda mrefu bila kuruhusu upepo upite ndani ni watapata fungus ukeni sawa na mwanaume anayevaa socksi zisizofaa kiafya. Chupi au socks zinazofaa ni zile za pamba au cotton.

Of course sababu za kupata ugonjwa wa fungus kwa mwanamke siyo tu kuvaa chupi inayobanaaaa kwa muda mrefu ni pamoja na kutawadha kwa kutumia maji ambapo maji hayo huacha unyevu ambao hutengeneza uvundo unaopelekea fungus ukeni.
Wanawake wengi hawajui kutawadha kwa kutumia maji. Wengi wamalizapo kujitawadha haja kubwa ndipo hurudi kujisafisha ukeni. Hii ni hatari sana kwani bacteria watokanao na kinyesi unawahamisha kutoka nyuma na kuwaleta mbele.
Mwanamke unapaswa kutawadha kwanza mbele kisha umalizie nyuma. 🐓🐕
Yaani hakikisha kuwa uchafu wa nyuma unaoweza kuwa umebakia kwenye vidole vyako usiuingize ukeni kwa namna yoyote ukijarib kuchunguza wanawake wengi hufuga kucha tena mkono wa kushoto iwje akitawadha uchafu usibaki kwenye kucha? tena kwa usahaulifu anajifashia mkono huo huo wenye kucha ndefu ambazo tayari zipo contaminated?. Tawadha pande zote lakini uhakikishe kuwa haviingiliani mbele na nyuma. Sawa dada yangu?? Uko poa hapo??
Kikubwa hapa ni usafi wa mbele na nyuma. Usafi wa chupi zetu. Uvaaji chupi wetu.
Kwa mfano uwapo safarini tena safari ndefu ya zaidi ya saa 8 ni vyema ukasafiri bila kuvaa chupi isipokuwa tu kama uko kwenye siku zile za adabu. Hata kama uko kwenye siku za adabu ni vyema ukasafiri bila kuvaa manguo mengi sana yanayobana mwili. Vaa chupi na sketi au suruali isiyoubana sana mwili wako.



3. Chupi husababisha ugumba kwa wanaume.

Sababu nyingi za ugumba tunaweza ukizipata kutoka kwa madaktari wetu wa hospitali zetu. Lakini kwangu mimi sababu nyingine ya ugumba wa wanaume kuwa ni kuvaa chupi zinazobana sana.
Mwanaume wengi siku hizi hawavai chupi. Anavaa kaptura au boxa badala ya chupi. Tena havai kaptura inayobana sana. Anavaa isiyobana viungo muhimu kwa uzalishaji wa watoto. Mbegu za kiume huzalishwa kwa wingi wakati wa baridi. Kuvaa chupi inayobana kwa muda mrefu husababisha korodani kuchemka sana na kushindwa kuzalisha mbegu nyingi. Mwanaume mwenye mbegu chache hushindwa kutungisha mimba kwani mbegu zake zinakwenda ukeni huku zikiwa dhaifu na kushindwa kuogelea ukeni.


4. Chupi husababisha miwasho sana kwenye mapaja ya mwanaume na mwanamke.

Epuka kuvaa chupi zinazobana ili kuepukana na miwasho.

Sunday, December 06, 2015

Kesi ya Rufaa ya Talaka ya Thadei Mtembei Imeahirishwa

wooden gavel and books on wooden table,on brown background

Na Mwandishi wetu

KESI ya rufaa ya madai ya talaka dhidi ya mfanyabiashara na Mkurugenzi wa shule ya sekondari ya St Mathew, Thadei Mtembei imeahirishwa baada ya wakili wa Mtembei, Mussa Kyoboya kudai mrufaniwa yuko India kwa matibabu.

Kesi hiyo inasikilizwa na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Temeke, Tarimo.

Katika kesi hiyo, mpeleka rufaa, Magreth Mwangu anawakilishwa na wakili Chacha Mrungu. Kesi hiyo ilikuja mahakamani juzi ambapo mrufaniwa alitakiwa kupeleka majibu ya rufaa.

Hata hivyo, wakili wake alisema majibu hayako tayari kwani kuna vipengele ambavyo alitakiwa kusaini, lakini ilishindikana kutokana na kuwa nchini India kwa matibabu. Kesi hiyo imepangwa kuendelea Desemba 16 mwaka huu.

Awali, kesi hiyo ilisikilizwa katika Mahakama ya Mwanzo Kizuiani mbele ya hakimu Rajab Tamaambele, ambapo Mwangu na watoto wake walionekana hawana haki, kwa madai sio mke halali na watoto hao ni wa zinaa kutokana na kuzaliwa nje ya ndoa.

Katika madai ya msingi, Mwangu anataka talaka, mgawanyo wa mali na matunzo ya watoto.

Katika sababu za rufaa, mrufani alieleza kusikitishwa na maamuzi yaliyotolewa na Mahakama ya Mwanzo Kizuiani Septemba Mosi mwaka huu, kwa hakimu kukosea kisheria kwa kutosaini nakala ya hukumu ikiwa ni pamoja na kukosekana kwa saini za wazee wa baraza.

Sababu nyingine ni Mahakama kukosea kisheria kwa kunyang’anya haki ya watoto kwa kutotoa matunzo ya watoto kwa mama, ambaye anaishi na mrufaniwa kwa miaka 20 na kuvunja Sheria ya Mtoto Namba 21 ya mwaka 2009. Maamuzi ya Mahakama ya Kizuiani yalishindwa kufuata sheria kwa wazee wa baraza kushindwa kutoa maoni yao.

Balozi Wilson Masilingi Aanza Ziara ya Kutembelea Vyama Vya Siasa DMV

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson Masilingi leo Jumamosi Desemba 5, 2015 alihudhuria mkutano wa Halmashauri ya CCM tawi la DMV ikiwa ni moja ya ziara zake anazotarajiwa kuzifanya kutembelea matawi ya vyama vya siasa nchiMarekani yenye lengo la kudumisha mshikamano na ushirikiano wa Watanzania bila kujali itikadi za vyama vyao.

Akiongea kwenye mkutano wa Halmashauri ya CCM DMV Mhe. Wilson Masilingi amesema lengo kuu ni kuwa karibu na vyama vya siasa kwa lengo la kuleta umoja na mshikamano ndani ya Jumuiya za Watanzania nchini Marekani na pia kuvitambua kama sehemu na sura ya Diaspora na kutoa wito kwa Watanzania waishio Marekani kuelekeza nguvu katika kuwekeza nyumbani bila kujali ufuasi wa chama unachoamini au kushabikia, wote ni Watanzania.

Mhe. Balozi Wilson Masilingi aliiomba Halmashauri hiyo ya CCM DMV kusaidia katika maendeleo ya Tanzania kwa kupanua wigo wao pamoja na kwamba lengo lao ni siasa na siasa ni sehemu ya maisha ya jamii na maendeleo ya jamii yanategemea siasa, kwa hiyo basi mnaposikia kuna muwekezaji yupo tayari kuwekeza Tanzania msisite Ubalozi upo wazi na utafanya kila liwezekanalo kuhakikisha muwekezaji huyo hapati vikwazo vyovyote.

Mwisho Balozi Wilson Masilingi aliwashukuru Watanzania kwa kuwa mabalozi wazuri nchini Marekani na kuwaasa kuishi kwa kufuata misingi na sheria za nchi ya Marekani.

 Mhe. Balozi Wilson Masilingi akiongea jambo na mwenyekiti wa tawi CCM DMV Bwn. George Sebo kwenye mkutano wa Halmashauri ya CCM DMV siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 mkutano uliofanyika Hampton Inn, College Park, Maryland. Picha na Kwanza Production/Vijimambo Blog
Mkutano ulianza kwa sala na kuwakumbuka wote waliotangulia mbele ya haki.

Mwenyekiti tawi la CCM DMV Bwn. George Sebo akifungua kikao cha Halmashauri ya CCM DMV kilichofanyika siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 katika ukumbi wa Hampton Inn, College Park, Maryland.

Saturday, December 05, 2015

Friday, December 04, 2015

Wanyonya Ume wa Mchungaji Wao Ili Wapone Maradhi Yao!

http://www.eurweb.com/wp-content/uploads/2013/02/valdesi-sobrino-picanto.jpg
Pastor Sobrino Valdeci Picanto wa Brazil
 
Mchungaji huko Brazil  Rev. Sobrino Valdeci Picanto, wa kanisa la pentecostal (walokole) aliwadanganya waumini wa kike kuwa wakinyonya ume wake (mboo) watafaidi maziwa maalum ambayo yatapona maradhi yao. Wengine aliwaambia watatajrika. Alisema kuwa ume wake unatoa maziwa enye nguvu na baraka kutoka kwa mwenyezi Mungu!  Alisema ni lazima dawa imwagwe mdomoni ndo iwe na nguvu.

Jamani, tangu lini maziwa ya baraka yanatoka kwenye ume? Sana sana utapata ugonjwa wa zinaa au mimba! Huyo jamaa alipenda anyonywe tu! Mchungaji Picanto yuko gerezani kwa kosa la ubakaji sasa.

Acheni kundangayika!

Kusoma habari kamili BOFYA HAPA!

Serikali Mpya ya Rais Magufuli! - Katuni


Saturday, November 28, 2015

Kumbe Kabaka Mwanga II wa Buganda alikuwa Shoga!

Papa Francis yuko nchini Uganda kwenye ziara rasmi. Alitoa heshima kwa wakristo 45 wailouawa huko Uganda zaidi ya miaka 100 iliyopita.  Katika historia, wanasema kuwa waAnglikana 23 waliuawa na waKatoliki 22 waliuawa kwa vile walitaka kusambaza ukristo Uganda.  Kumbe waliuawa kwa vile Kabaka huyo alikuwa shoga na hao wakristo walikataa kutembea naye! Duh! Kabaka anataka uroda halafu unamnyima! Walivyomnyima ilikuwa kashfa kwake!

Sasa, tunaweza kuona sababu kuu ya waGanda kuwa na sheria kali dhidi ya usenge/ushoga.   barani Afrika wao wako wazi kabisa na chuki ya dhidi ya ushoga. Ni historia ambayo hawapendi kuongelea. (Zamani  kabla ya mamisionari ushoga/usenge ulikuwa ruksa!)




******************************************************
By NICOLE WINFIELD and RODNEY MUHUMUZA
Associated Press

   NAMUGONGO, Uganda (AP) - Pope Francis on Saturday honored the Ugandan Christians who were burned alive rather than renounce their faith a century ago, urging today's Catholics to follow in their missionary zeal and spread the faith at home and abroad.

   A somber Francis prayed at shrines dedicated to the 23 Anglican and 22 Catholic martyrs who were killed between 1885 and 1887 on the orders of a local king trying to thwart the influence of Christianity in his central Ugandan kingdom. According to historians, the Christians were also killed because they refused the king's sexual advances, citing the church's opposition to homosexuality.

   At Namugongo, outside the capital, Kampala, where most of the martyrs were burned alive, Francis prayed first at the gruesome sanctuary dedicated to the Anglicans, kneeling before part of the same tree where they were tortured before being executed. He then prayed at the Catholic shrine and celebrated Mass in their honor to mark the 50th anniversary of the Catholics' canonization.

   As many as 2 million people were expected to attend the Mass, including Ugandan President Yoweri Museveni, the president of South Sudan and the descendant of the king who ordered the deaths.

   Francis urged them to use the martyrs' example of faith to be missionaries at home by taking care of "the elderly, the poor, the widowed and the abandoned."

   "This legacy is not served by an occasional remembrance or by being enshrined in a museum as a precious jewel," he said. "Rather we honor them and all the saints when we carry on their witness to Christ, in our homes and neighborhoods, in our workplaces and civil society, whether we never leave our homes or we go to the farthest corner of the world."

   The Argentine pope knows of what he speaks. When he joined the Jesuit order as a young man, he longed to be a missionary in Japan. But his superior told him to stay home for health reasons, and he later developed a ministry in the slums of Buenos Aires that has formed the basis of his papacy.

   During his two days in Uganda, Francis is expected to touch on some of the same themes he emphasized during the first leg of his trip in Kenya: corruption, poverty and giving young Christians hope and encouragement. After the Mass on Saturday, Francis has a rally with young people, a visit to a charity and a meeting with local priests, seminarians and nuns on his agenda.

   Some of the pilgrims attending the Mass had been here all night to honor the martyrs and see the pope, braving rains and sleeping on mats to guard against the mud that turned the grounds into chocolate-colored muck.

   "They are so important because they sacrificed their life because of their religion," said Beneh Ssanyu, 27, who showed off the mud encrusting her sandals and pants - evidence of her arrival at 1 p.m. Friday that scored her a prime front-row seat.

   Security at the shrine was tight, with those entering the main area passing through metal detectors and police boats monitoring the moat surrounding the altar where Francis celebrated the service.

   Francis has made a point on his foreign travels to honor local martyrs in hopes of inspiring a new generation of missionaries. When he was in South Korea, for example, he beatified 124 missionaries who helped bring the faith to the Korean Peninsula. He has also spoken out frequently about today's martyrs, the Christians in the Middle East and Africa who have been slaughtered by Muslim militants.

   The history of Uganda's martyrs has helped shape the Catholic Church here, with huge numbers of pilgrims flocking to the Namugongo shrine, many of them Africans arriving from as far away as Congo and Tanzania. Most of the pilgrims walk long distances to the site to underscore their faith.

   King Mwanga II of Buganda Kingdom ordered the martyrs killed during a period of political and religious turmoil as he tried to assert his authority amid the growing influence of missionaries from Europe.

   But the history of the martyrs also shows a personal grudge Mwanga held against them: After the martyrs converted to Christianity, they began rebuffing his sexual advances since church teaching forbid homosexuality - a humiliation that was part of the reason they were ordered killed, according to the history of the killings, "African Holocaust" by J.F. Faupel.

   "It is absolutely true. It is a fact," said Bishop Giuseppe Franzelli, a longtime Italian missionary in Uganda. "When they became Christians, they saw that this was not according to the Gospel, the teaching of Christ and they said no."

   The little-known history might help explain why homosexuality remains so taboo today in Uganda, which is 47 percent Catholic and has criminalized homosexuality.

   The Vatican has refused to say whether Francis will discuss gay rights openly while here.

   On Sunday, Francis heads to his final destination, the Central African Republic.




Mashoga wakitafuta wateja katika hoteli ya kitalii

Friday, November 27, 2015

Waziri Mkuu Majaliwa Aamuru Maafisa Kadhaa wa TRA Kukamatwa

Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa leo ameamuru kukamatwa kwa maafisa kadhaa  wa Mamlaka ya Mapato (TRA) na wengine kufukuzwa kazi  baada ya kufanya ziara ya kushtukiza Bandarini na kukuta madudu ambayo hakuyafurahia.
Maafisa hao, ambao kwa sasa tunahifadhi majina ili Jeshi la Polisi liweze kuwashughulikia, wametakiwa pia kusalimisha hati zao za usafiri.
Hii imekuja baada ya kugundulika kwamba kuna makontena 349 yenye thamani ya zaidi ya bilioni 80 ambayo data za Mamlaka ya Bandari inazo lakini katika mtandao wa TRA hayaonekani.
Habari kamili inaandaliwa. Fanya subira....
Kwa sasa anza na picha....


Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na uongozi wa TRA na TPA alipofanya ziara ya kustukiza Bandarini leo asubuhi.
 Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akiongea na viongozi wa TRA na TPA
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akikabidhi orodha ya makontena yaliyopotea na ambayo TRA haina taarifa nazo
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa 
akiagana na viongozi wa TRA na TPA.


Thursday, November 26, 2015

Saturday, November 21, 2015

Kanisa za WaKenya Boston Zimeguezwa Miradi ya Kutafuta Pesa

 
Pastor Elizabeth Wanyoike of the newly launched International Restoration Reformed Church (IRRC) in Tewksbury, near Lowell during dedication ceremoney on Sunday November 15, 2015. AJABU MEDIA PIC/H.MAINA
 
Kenyan Churches in Boston turned into financially motivated Social Clubs, says new Pastor
 
LOWELL, Mass.,( Ajabu African News) Nov 19__Most Kenyan community churches in Boston have abdicated their primary role of spreading the true gospel of Jesus Christ and instead have been turned around into "help those who help you" social clubs emphasizing too much on financially motivated manipulations. 
The charge was made by pastor Elizabeth Wanyoike last Sunday during the dedication ceremony of the newly launched International Restoration Reformed Church (IRRC) in Tewksbury, near Lowell.

She said that many Kenyans attending Kenyan community churches today have no clue of where they are headed yet they are being lead down the drain by church leaders many of whom are only concerned with parishioner contributions to cater for their weekly paychecks and social problems among members. 

"There is a lot of ungodliness in the church today.The church has been turned around to help those who help you. It is the spirit of Jezebel and somebody must wake up to breaks the yokes of this spirit," she said during the sermon top about a dozen Kenyans present"

It is time to destroy the ungodliness in our church just like Elijah destroyed the idols that citizens were worshipping during King Ahab's rule," she added while quoting from the book of1st Kings Chapter 16 &17.

.Wanyoike said that there is a spirit of fear, oppression and intimidation going around the body of Christ today in the Kenyan community similar to what took place during King Ahab's reign.

"You can be in the church but the people in authority are taking you nowhere. People are covered in the spirit of oppression and intimidation."
She called on Kenyans of faith to take a proactive effort to change things so that the church "can operate on what God wants us to do."

"Things have to change and the church return to order. We don't have to gather for the sake of gathering. Even Obadiah was so afraid to tell the King that Prophet Elijah had arrived with a message to the people but Elijah forced him to bring up King Ahab to listen to the message and destroy the alters of worshiping idols instead of the read God," she added.

Fedha za Hafla ya Bunge Zinunue Vitanda Muhimbili: Rais Magufuli

Baada ya kulihutubia na kulizindua bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt JOHN POMBE MAGUFULI amehudhuria hafla fupi iliyoandaliwa kwa ajili ya wabunge katika viwanja vya Bunge Mjini Dodoma na kuagiza fedha zilizochangwa kwa ajili ya kugharamia hafla hiyo zipelekwe Katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya kununulia vitanda vya wagonjwa.

Mheshimiwa Magufuli ametoa agizo hilo baada ya kupokea taarifa kuwa wadau mbalimbali wamechanga kiasi cha shilingi milioni 225 kwa ajili ya kugharamia hafla ya wabunge katika siku ya uzinduzi wa Bunge.

Dkt Magufuli amesema alipata taarifa za kuwepo kwa michango hiyo ya fedha na kutoa maelekezo kuwa zitumike kwa kiasi kidogo kwa ajili ya hafla hiyo na sehemu kubwa zipelekwe katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ili zikatumike kununulia vitanda na hivyo kupunguza tatizo la wagongwa wanaolala chini kutokana na uhaba wa vitanda unaikabili hospitali hiyo.

“Nilipoambiwa kwamba zimechangwa shilingi milioni 225 zimekusanywa kwa ajili ya sherehe, nikasema fedha hizo zipelekwe katika hospitali ya Taifa Muhimbili zikasaidie kununua vitanda” alisema Dkt Magufuli na kusisitiza kuwa “kwa kufanya hivyo tutakua tumejinyima sisi wenyewe lakini tutakua tumewanufaisha wenzetu ambao wanamatatizo makubwa yanayoweza kutatuliwa kwa fedha hizo”.

Awali akitoa taarifa ya michango hiyo Ofisa wa Spika wa Bunge Bwana SAID YAKUBU amesema jumla michango iliyopatikana na shilingi milioni 225 na kwamba fedha zilizotumika katika hafla hiyo ni shilingi milioni 24 tu baada ya kuzingatia maagiza ya Rais Magufuli.

Katika Hafla hiyo Rais Magufuli amekabidhi vyeti vya kutambua mchango wa wadau waliochangia fedha wakiwemo Benki za NMB, CRDB na Benki ya Afrika pamoja na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya PSPF na PPF.

Gerson Msigwa

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano IKULU

November 20, 2015

USA Visa Waiver Program

Visa Waiver Program

Fact Sheet
Office of the Spokesperson
Washington, DC
November 20, 2015



The Visa Waiver Program (VWP), administered by the Department of Homeland Security (DHS), allows eligible citizens or nationals of countries which have met U.S. security requirements to travel to the United States without visas in exchange for visa-free travel to those countries by U.S. citizens. The VWP utilizes multiple layers of security to detect and prevent terrorists, serious criminals, and other potentially dangerous individuals from traveling to the United States. These layers of security include comprehensive screening of VWP travelers prior to departure for the United States, at various points throughout the traveler’s journey, and upon arrival at U.S. ports of entry.
Over the last year, DHS and the Department of State, in coordination with several other federal agencies, have made a number of significant enhancements to the VWP to ensure our security apparatus continues to adapt in the face of evolving threats.
How Does the Visa Waiver Program Work?
  • Every prospective VWP traveler undergoes counterterrorism screening and must receive approval through DHS’ Electronic System for Travel Authorization (ESTA). Through ESTA, DHS evaluates whether individuals are eligible to travel to the United States under the VWP before they are allowed to board a carrier bound for the United States.
  • The counterterrorism check draws on information from U.S. law enforcement and intelligence agencies. DHS uses this information to decide if the travel poses any law enforcement or security risks. Without DHS approval through ESTA, VWP travelers cannot travel to the United States and must appear in person for a visa interview if they still want to travel to the United States.
  • Any individual applying for a U.S. visa undergoes thorough biographic and biometric screening against U.S. law enforcement and counterterrorism databases. Biometric screening includes checks based on fingerprints and/or facial recognition software. No visa can be issued unless all relevant concerns are fully resolved.
  • Information submitted during an ESTA application is shared with consular officers to help them determine whether a visa should be issued after an ESTA application has been denied.
  • As part of this screening process, information that identifies suspected or known violators of the law and other persons of concern will be provided to the appropriate law enforcement, national security, and/or counterterrorism agency.
  • This process has been enhanced repeatedly to improve security and more effectively identify individuals who might pose a threat to the United States.
  • Travelers must be a citizen of a VWP country to use the program. Residence in a VWP country, or the possession of refugee travel documents issued by a VWP member state, does not qualify an individual for VWP travel.
  • For the list of countries whose citizens are eligible for VWP travel, please visit http://travel.state.gov/content/visas/en/visit/visa-waiver-program.html.
Recent Enhanced Security Measures
  • DHS, in consultation with the Department of State, continuously adapts the VWP to address current threats.
o DHS introduced additional data fields to the ESTA application in November 2014 that already have already security benefits.
o DHS introduced new traveler screening and information sharing requirements for VWP countries in August 2015 specifically to address the threat posed by foreign terrorist fighters.
o DHS and the Department of State are working with VWP partners to implement the new VWP requirements, which will strengthen U.S. security and the security of our partners.
  • These security enhancements are part of our continuing assessments of U.S. security in the face of evolving threats and challenges, and our determination to stay one step ahead of those threats and challenges.
For further information, please contact the Bureau of Consular Affairs at CAPressRequests@state.gov or visit travel.state.gov.

Thursday, November 19, 2015

Mwanahabari Nashon Kenedy Awapa Siri Ya Mafanikio Wasanii wa Mwanza

Kulia ni Mwanahabari Nashon Kenedy kutoka gazeti la kiswahili la Habari Leo na lile la kiingereza la Daily News akiongea katika hafla ya kuzaliwa kwa Yusuph Kisiba a.k.a Yuskiss ambae ni Mtengenezaji wa Filamu katika Kampuni ya Shafineyz Film Production ya Jijini Mwanza.
Na:George Binagi-GB Pazzo wa Binagi Media Group
Mwanahabari Nashon Kenedy kutoka gazeti la kiswahili la Habari Leo na lile la kiingereza la Daily News amewashauri wasanii wa maigizo Jijini Mwanza, kubadilika na kuigiza filamu zinazogusa maisha halisi ya Kitanzania na kuachana na uigizaji wa filamu zisizo na uhalisia wa maisha ya Kitanzania hususani filamu za mapenzi. 

Kenedy aliyasema hayo jana katika hafla ya kuzaliwa kwa Yusuph Kisiba a.k.a Yuskiss ambae ni Mtengenezaji wa Filamu katika Kampuni ya Shafineyz Film Production ya Jijini Mwanza ambapo alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo ambayo pamoja na wageni wengine, pia ilihudhuriwa na wasanii mbalimbali wa muziki na filamu kutoka Jijini Mwanza.

"Japokuwa maisha yetu yanategemea mapenzi, lakini mimi nawashauri kwamba acheni kuigiza filamu za mapenzi kila siku kama mnahitaji kufanikiwa. Igizeni filamu zinazoeleza maisha halisi ya kitanzania kama vile kuonyesha matatizo yanayowakabili wananchi, na hapo ndipo mtaweza kuwa tofauti na waigizaji wengine jambo ambalo litawasaidia kufikia katika mafanikio yenu". Alibainisha Kenedy.

Katika hafla hiyo, Kisiba aliwashukuru wale wote walioungana nae katika kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa ambapo aliahidi kuitimiza ahadi yake ya kuhakikisha kuwa soko la uigizaji wa filamu Jijini Mwanza linafufuliwa kupitia Kampuni anayofanyia kazi ya Shafineyz Film Production kwa kuwa ni aibu kukosekana kwa soko la filamu Jijini hapa ikilinganishwa na majiji mengine nchini kama vile Jiji la Dar es salaam. 
Tazama HAPA Picha za Hafla hiyo

Wednesday, November 18, 2015

Mwanalibeneke Yuskiss Kisiba Asherekea Birthday!


Anaitwa Yusuph Kisiba a.k.a Yuskiss Kisiba ambae ni Blogger @Lake Zone Media & Kisibasharesky Media, Graphics Desiner & Video Editor @Shafineys Film Production Jijini Mwanza.
Na:George Binagi-GB Pazzo wa Binagi Media Group
Tarehe kama ya leo (Nevemba 19) miaka kadhaa iliyopita alizaliwa hivyo hii leo anafurahia siku yake ya kuzaliwa na ndugu, jamaa na Marafiki. Nasi tunamtakia maisha mema katika kuzaliwa kwake.

"Novemba 19 ni tarehe ambayo Mwenyezi Mungu aliweza kuniruhusu kutoka katika tumbo la mama yangu kipenzi na kuuona ulimwengu huu. Na hapo ndipo safari yangu ilipoanzia na ikawa ndiyo chanzo cha kufahamiana na wewe hivi sasa. Novemba 19 ni siku ambayo huwa ya kipekee sana kwangu katika huzuni na furaha kutokana na kuishi mazingira haya ya ulimwengu uliojaa kila aina ya uzuri na ubaya wake.Ukiwa kama ndugu/rafiki yangu sina budi kukukumbusha kuungana nami kufanya ibada ikiwa na lengo moja la kumuomba  Mungu atusamehe makosa yetu. Kwa yeyote niliewahi kumkosea sina budi kukuomba radhi katika siku hii". Anasema Kisiba.

Monday, November 16, 2015

Msaada wa Wasamaria Wema Unahitajika Kwa Ajili ya Matibabu

Ndugu Wasamaria wema
Napenda kutumia fursa hii kukushirikisha habari ya kusikitisha kuhusu dada Joyce Mwambepo (pichani akiwa na mwanaye, na migu yake iliyopooza) mkaazi wa Sinde jijini Mbeya. Dada huyu mwenye umri wa miaka 27 anaishi na bibi yake mwenye umri wa miaka 80 pamoja na mwanaye mwenye umri wa miaka 4.
Kwa bahati mbaya mwezi April mwaka jana dada huyu alipata ajali ya kugongwa na gari ambayo haikusimama kumsaidia. Ila kwa msaada wa wasamaria wema alipelekwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa  Mbeya ambako inasemekana alikaa kwa miezi mitatu bila kupata matibabu.
Katika uchunguzi wa awali ilibainika kuwa Joyce amevunjika miguu yote miwili,  hivyo akahamishiwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili ambako pia baada ya kukaa kwa miezi kadhaa alirejeshwa Mbeya baada ya kukosa shilingi 550,000/- za vipimo na matibabu.
Hadi nakutana naye dada huyu alikuwa amelala nyumbani kwa bibi yake (pichani kushoto) ambaye ni mlezi wake tangu akiwa na miaka minne baada ya wazazi wote wawili kufariki dunia. 
Hawezi kukaa wala kusimama na anajisaidia hapo hapo kitandani kwa msaada wa mwanaye na bibi yake. Inasikitisha.
Hivyo nimejitahidi kufuatialia ili kujua mahitaji halisi lakini sikufanikiwa kumpata daktari bingwa wa mifupa . Ili kumsaidia Joyce inatakiwa aanze process upya za matibabu kuanzia hapa Mbeya referral Hospital  hadi Muhimbili jijini Dar es salaam.
Gharama za matibabu ni kama ifuatavyo:
1. shilingi 300,000/- za kupima CT-SCAN
2. Shilingi 250,000/- za MRI
3. Usafiri wa kutoka Mbeya-Dar kwa gari maalum la kukodi 700,000/-
4. Gharama za msaidizi ambaye ni rafiki yake 300,000/-
5. Chakula 450,000/- (Endapo watakaa hospitali mwezi mzima)
6. Gharama za matibabu (CT-SCAN&MRI ni vipimo tu) 500,000/-
7. Na mahitaji mengineyo wakiendelea kupata tiba 500,000/-

Hivyo kwa kuanzia kiasi cha shilingi 3,000,000/- (milioni tatu) kinahitajika kumpunguzia mateso dada yetu huyu. Asante sana kwa moyo wako wa kujitoa na Mungu atakubariki.

Deo Kakuru Msimu
Msamaria mwema
+255769 512 420

Wakati huo huo kwa niaba ya Michuzi Media Group, Ankal amejitolea kusaidia uratibu wa kufanikisha matibabu ya dada Joyce. Hivyo unaweza kuwasiliana naye kwa email issamichuzi@gmail.com ama whatsapp namba +255 754 271266 kwa jina la Ankal.

Saturday, November 07, 2015

Kizee wa Miaka 72 Aolewa na Kijana wa Miaka 22


Wadau, kijana wa miaka 22 kutoka Dominican Republic, amemwoa bi kizee tajiri wa kiMarekani mwenye miaka 72.  Ni mapenzi au.... labda kizee anapenda ngono anayopata kutoka kwa huyo kijana, na huyo kijana anataka hela ya huyo bi kizee na pia atapata makaratasi ya kukaa Marekani.  Haya tuwatakie maisha mema ya ndoa.