Saturday, March 18, 2017

Comfort Zone - A Poem by Prof Richard Mabala

FROM FACEBOOK

Comfort Zone

By Richard Mabala 

First they came for the big guys
They were all fisadis
But I am not a fisadi so why should I speak out?
Even if no evidence has been given against them
We were told they were fisadis
What greater evidence do you want?
Silently I applauded.
Then they came for the artists
Decadent artists leading immoral lives
Why should I support them?
No evidence again but God had spoken
I said not a word.
Of course they came for the gays
Even wanted to publicly declare their names
Even more disgusting than the artists
I don't care whether they do it in private or not
They deserve it.
No need to speak out
They also came for the activists
Those arrogant unelected nobodies
Pushing their own agendas as if they were the people's choice
They had to be silenced
So silent I remained.
Then they came for an Asian
These Asians, don't we know them
They are just exploiting us
How can he claim to be a citizen like me?
A proud Tanzanian
So what if he was a councillor in my own party
Why should I speak for these exploiters?
And anyway I support that other team
Too patriotic to support him or his team.
So no need to speak out
Even if there seems be a vendetta against him
For daring to threaten the son of God
Silence is golden
Then they came for the opposition.
Why should they go on politicking even after the election.
Throw them in jail
And keep them there to show our leaders brook no opposition
Opposition disrupts their good intentions.
Troublemakers.
They deserve to stay in jail
I said nothing
The same is true of those people
Who used unbecoming language
On Facebook
They should have known better
They were warned
But still the persisted.
Why should I speak in their favour
Then they came for the lawyers
Especially those dumb oppositionist lawyers
Wanting to take over their association
And become activist
Activist? Really?
We know those lawyers are just after money
And power
Corrupt.
Surely they can defend themselves anyway.
Say nothing.
Then they came for their own party members
Ha ha ha. You see their foolishness
Fraternising with the enemy when politics is no longer about adversaries
But enemies.
They couldn't even see which way the wind is blowing
And bow before it
They were flattened
And I will never say a word
Even if they belonged to my party
Unlike them, I am loyal
Always loyal.
But hang on
What are those boots outside my door?
What have I done?
HELP! Will someone speak out for me?
I have done nothing.
Why the silence?
Am I the only one left?

Mbinu Hizi zitakusaidi Kukabiliana na Mvua Jijini Dar es Salaam

Na Jumia Travel Tanzania

Hivi kuna mkazi yeyote wa jiji la Dar es Salaam ambaye ni mgeni wa adha zitokanazo na mvua zinazonyesha? Sidhani kama kuna mtu yeyote hafahamu ya kwamba mvua ikinyesha kutakuwa na foleni zisizokwisha, barabara na mitaa tofauti jijini kujaa maji, mafuriko na matamko kadha wa kadha kutoka kwa viongozi wa serikali kuwataka wananchi wahame mabondeni.

Lakini ni wangapi wametafakari watawezaje kukabiliana na mvua zitakaponyesha? Zipo mbinu nyingi tu ambazo Jumia Travel inakushauri uzizingatie ili kipindi cha mvua nyingi za Dar es Salaam kwako kiwe ni cha kawaida katika mwaka. 


Amka mapema kukabiliana na foleni ili uwahi shughuli zako
Hakuna wakati ambao kunakuwa na foleni kubwa na zisizopungua kwa muda mrefu jijini Dar es Salaam kama kipindi cha mvua! Lakini jambo hili sio la kushangaza kwa sababu kila mwaka hali hii inajirudia. 

Na hiki ni kipindi ambacho mabosi wengi huchukia sana pengine kuliko vipindi vyote vya mwaka maana visingizio vya wafanyakazi wao kuchekelewa kazini kwa sababu ya mvua huwa haviishi. Kwa hiyo unakabiliana vipi na hali hiyo? 

Kwanza kabisa lazima uwe makini katika kuwahi kuamka mapema na pia njia ya usafiri utakayoitumia. Inakubidi kuwahi kuamka mapema sana kama unategemea usafiri wa umma au binafsi. Kwa sababu ukifanya hivyo kama kutakuwa na foleni barabarani basi utaziwahi ukilinganisha na ukichelewa kuingia barabarani. Lakini pia kama unategemea usafiri wa umma, mabasi ya mwendokasi ni mkombozi mkubwa kwenye kipindi hiki. Hivyo kwa maeneo ambayo usafiri huu unapatikana ni vema kuutumia ipasavyo kwa sababu yenyewe hayakai foleni kutokana na kuwa na njia zao pamoja na kupewa kipaumbele.    

Nunua vifaa vya kujikinga na mvua
Kutokana na jiji la Dar es Salaam kuwa na vipindi virefu vya jua na joto kali, imekuwa ni nadra sana kuwakuta wakazi wake wana vifaa vya kujikinga na mvua kama vile mwamvuli, koti, sweta au viatu vya mvua. Inashauriwa kuwa na vifaa hivi nyumbani kwako ili kujikinga ifikapo kipindi cha mvua na sio kuanza kufikiria kununua kwani inawezekana usiwe na bajeti hiyo pindi unapovihitaji. Vifaa hivyo ni muhimu kwani hukukinga na baridi, kutolawana, magonjwa na hata kutunza mavazi yako kutokana na maji ambayo huweza kusababisha kuharibika.
Umakini kwenye chombo chako cha usafiri 
Kwa wenye vyombo vya usafiri wanajua wenyewe ni kadhia gani wanayokumbana nayo ikifika kipindi cha mvua. Kipindi hiki ni jambo la kawaida kukuta magari kadhaa yamezimika au kukwama barabarani kutokana na sababu mbalimbali za kiufundi. Lakini pia barabara nyingi huharibika na kutopitika kabisa hivyo kulazimisha chombo chako kupita ni kujitafutia kuingia gharama zisizohitajika siku za usoni. Kama inawezekana tafuta njia mbadala ya usafiri katika kipindi hiki au pita kwenye njia ambazo una uhakika ni salama kwa chombo chako.

Kuwa makini na vifaa vyako vya umeme
Siyo vifaa vyote vya umeme vimetengenezwa vikiwa na uwezo wa kuzuia maji kutokuingia ndani yake. Licha ya makapuni mbalimbali kuja na teknolojia hiyo lakini unashauriwa kuwa makini sana aidha kwa kuvivika vifaa maalumu vya kuzuia maji au kuvikinga kabisa na maji. Kipindi hiki ndicho ambacho wengi hupatwa na majanga ya kuharibikiwa na simu, kompyuta, radio pamoja na luninga huko majumbani.

Kuwa makini na vyakula utakavyokula
Kama huwa unakuwa makini na aina ya vyakula unavyokula basi kipindi hiki inabidi uwe makini zaidi. Mvua zikinyesha jijini Dar es Salaam ndiyo kipindi ambacho pia kunakuwa na mlipuko wa magonjwa kadha wa kadha kama vile kipindupindu. Inashauriwa kula chakula sehemu ambayo unaiamini na inayozingatia usafi wa hali ya juu au kama inashindikana uwe unabeba chakula unachopika mwenyewe au kutokula kabisa.  

Tumia muda wako kusoma vitabu
Sio watu wote wana utaratibu wa kusoma vitabu kwenye siku zao za kawaida badala yake wanatazama filamu, kusikiliza muziki, kutoka wikendi au kupendelea kutembea. Lakini katika kipindi hiki ambacho mvua zinanyesha, barabara hazipitiki, hali ya hewa ni baridi na sehemu nyingi za starehe au kutembelea zinakosa watu ni vema ukajaribu kusoma vitabu. Amini usiamini kuwa hata kutazama filamu na kusikiliza muziki hufikia mahala vinachosha, hiki kinaweza kikawa ni kipindi kizuri cha kujaribu kitu tofauti, nunua vitabu na usome ili uongeze maarifa. 

Hivyo basi tusiifanye mvua ikawa ni kisingizio cha kutofanya shughuli zingine au majukumu mengine yanayotukabili. Kila kipindi huja na changamoto pamoja na fursa zake, ni vema kupambana nazo na kuzitumia ili kusonga mbele.

Dk. Ryoba Awaona Waanidshi wa Habari wa Uhuru Leo

DK. AYUB RIOBA AWANOA KWA SEMINA YA WELEDI WAANDISHI WA HABARI WA GAZETI LA UHURU, JIJINI DAR ES SALAAM, LEO
 Mwandishi wa habari nguli wa siku nyingi,Dk. Ayub Ryoba, akiendesha semina ya kunoa weledi wa taaluma ya uandishi wa habari kwa waandishi wa habari na baadhi ya watumishi wa Kampuni ya Uhuru Publications Ltd, Wachapishaji wa Magazeti ya Uhuru, Mzalendo na Burudani, leo katika Ukumbi wa Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam. Dk. Ryoba ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), ana shahada ya Udaktari wa Falsafa (PhD) katika Sayansi ya Jamii aliyoipata katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 Mwandishi wa habari nguli wa siku nyingi,Dk. Ayub Ryoba, akiendelea kutoa 'nondoz' kwa wafanyakazi hao wa UPL, huku wafanyakazi hao wakimsikiliza kwa makini sana
 Mwandishi wa habari nguli wa siku nyingi,Dk. Ayub Ryoba, akifafanua mada zake kwenye semina hiyo ya kunoa weledi wa kitaaluma
 Washiriki wa semina hiyo wakiwa ukumbini
 Dk. Ayub Ryoba, akiendelea kutoa mada kwenye semina hiyo
 Washiriki wakifuatilia kwa makini mafunzo ya Dk. Ryoba
 Yassin Kayombo (aliyesimama) akijitambulisha kwa Ryoba (kulia) na kwa washiriki wengie wa semina hiyo
 Mgaga akijitambulisha
 Jongo akijitambulisha
 Mnkondo akijitambulisha
 Ally akijitambulisha
 Furaha Omari akijitambulisha 
 Gailanga akijitambulisha
 Utambulisho ukiedelea
 Utambulisho ukiendelea
 Washiriki wakiwa ukumbini
 Dk. Ryoba akiendelea na semina hiyo
 Washiriki wakiwa katika kundi la kwanza kujadili mada
 Washiriki katika kundi la pili kujadili mada
 Washiriki katika kundi la tatu kujadili mada
 Washiriki kundi la nne wakijadili mada
 Dk Ryoba akipitiapitia mada zake wakati akisubiri mrejesho wa maswali aliyowapa washiriki 
 Dk. Ryoba akijadiliana jambo na baadhi ya washiriki wa semina hiyo wakati wa mapumziko. Kulia ni Furaha Omar na Bashir Nkoromo
 Dk. Ryoba akijadiliana jambo na baadhi ya washiriki wa semina hiyo wakati wa mapumziko. Kulia ni Furaha Omar na Bashir Nkoromo
(PICHA ZOTE NA KAMERA YA BASHIR NKOROMO)

Saturday, March 11, 2017

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utallii Yatembela Eneo lenye Mgogoro la Por Tengefu la Loliondo

Msafara wa Magari ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi,Malisili na Utaalii,yakpita katika maeneo mbalimbali ya Pori Tengefu la Loliono kwa ajili ya kujionea hai halisi ya mgogoro ulioo katika eneo hilo.
Mwenyekii wa Kamati ya Kudumu ya Ardhi ,Maliasii na Utalii,Atashasta Ndetiye (katikati) akiongozana na wajumbe wengine wa kamati hiyo kutizama vyanzo vya maji vilivyoko katika Pori Tengefu la Loliondo.
Waziri wa Malisili na Utalii ambaye pia ni mjumbe wa kamati hiyo,Prof Jumanne Maghembe akiongozana na wataalamu katika ziara ya kamati hiyo.
Mtafiti Mkuu wa Idara ya Ikolojia (TAWIRI) Dkt Edward Khoi akitoa maelezo ya kitaalamu kwa wajumbe wa kamati ya kudumu ya Ardhi,Malisili na Utalii wakati wakitembela Pori tengefu la Loliondo.
Baadhi ya wajumbe wa kamato hiyo wakifuatilia maelezo kutoka kwa wataalamu wa Ikolojia na Uhifadhi.
Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti,William Mwakilema akiwaeleza wajumbe w kamati hiyo madhara yatakayojitokea endapo eneo la Pori Tengefu la Loliondo halita hifadhiwa.
Wajumbe wa Kamati ya Maliasili na Utalii,wakitizama eneo linalotajwa kutengenezwa na wafugaji kwa ajili ya kunyweshea maji mifugo yao ndani ya Pori Tengefu la Loliondo.
Eneo linalouiwa na wafugaji unyweshea mifgo yao.
Sehemu ya Mabirik yanayotajwa kutengenezwa na jamii ya wafugaji kwa ajili ya kunywesha mifgo yao.
Mwenyekiti a Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi,Maliasili na Utalii,Atashsta Ndetiye (kulia) pamoja na Waziri wa Malisili na Utalii,Prof ,Jumanne Maghembe wakitizama eneo ambalo i mapiio ya maji katik Pori Tengefu la Loliondo.
Moja ya Makundi ya Ng'ombe yaliyokutwa na Kamati hiyo katika Pori Tengefu la Loliondo.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi,Maliasili na Utalii wakizungumza na mmoja wa wafugaji waliokutwa wakichunga Ngombe ndani ya Pori Tengefu la Loliondo. 
Kamati ilikutana pia na Changamoto ya uboovu wa Miundombinu ya barabara hali iliyolazimu magari kupita kwa tahadhari .
Wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi,Maliasili na Utalii wakitizama moja kati ya vyanzo vy maji vinavyotiririsha maji yake katika mto Gurumeti uliopo katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Mbunge wa Jimbo la Sumve ambaye pia ni mjube wa kamati hiyo,Richard Ndasa akizungumza jambo mara baada ya kutizama moja ya vyanzo vya maji vilivyoko katika eneo la Pori Tengefu la Loliondo.
Sehemu ya Makundi ya Mifugo pamoja na Mashamba yaliyopo katika eneo la Pori Tengefu la Loliondo.


Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazinia